2013-02-20 15:42:34

Maoni mbalimbali ya Makardinali juu ya Kjiuzuru kwa Papa Benedikto XV1


Viongozi wa Kanisa wa ngazi za juu , wanaendelea kutoa maoni yao juu ya maamuzi ya Papa Benedikto XV1, kujiuzuru hapo tarehe 28 Feburari 2013.
Kardinali Julian Herranz, Mtaalam wa sheria za Kanisa, akitoa maoni yake anasema, kwanza alipata mshituko mkubwa wakati Papa akitangaza maamuzi yake. Lakini mara, alipata hisia tofauti , hisia ya furaha ndani mwake, kwa unyenyekevu na upendo, ulionyeshwa Papa kwa Kanisa .
Kardinali Herranz alieleza hayo wakati akizungumzia kustaafu kwa Papa katika mahojiano na gazeti la El Paris , na kuchapishwa siku ya Jumanne. Alisema, kibinadamu , mara baada ya kusikia maamuzi ya Papa alipatwa na hisia hizi za kusikitika, hasa alipotupa fikira zake katika miaka ya nyuma, wakati alipofanya kazi bega kwa bega na Josef Ratizinger kablaya kuwa Papa.

Na amemshuhudia kwamba, Papa Benedikto XV1, si tu mtaalum mkubwa teolojia, lakini pia ni mtu mwenye kuwa na imani kubwa isyokuwa ya kawaida kwa Kristu, imani anayopenda kuifikisha kwa watu wote , kwa unyenyekevu, na hivyo si tu kupitia nguvu za mamlaka siku zote, lakini pia katika maisha ya kawaida.

Na kama Mwanasheria anasema, maamuzi ya Papa yamefanyika kwa mujibu wa sheria ya kanisa namba 332, kipingere cha 2. Hivyo Papa hajaenda nje ya sheria za Kanisa, kama wengine wanavyofikiri. .

Na Kardinali Jean-Louis Tauran, katika mahojiano na Antoine-Marie Izoard wa gazeti la "Insider Vatican," alielezea zaidi juhudi zinazofanywa na Papa katika siku za hivi karibuni katika kwenda sambamba na kishindo cha mawasiliano jamiii.Amesifu kwamba, juhudi hizo, zimewezesha wengi kutazama kwa makini zaidi, jinsi ya kukabiliana na changamoto kubwa katika dunia ya kisasa. Pamoja na uchaguzi wake - aliongeza - ametuonyesha jambo lisilokuwa la kawaida la uwepo wa nguvu ya ndani isiyokuwa na kipimo.
Nae Askofu Mkuu Christoph Schönborn, Austria katika gazeti la Austria la "Profil" akinukuliwa pia na gazeti la "Corriere della Sera" matoleo ya Februari 19, anasema kujiuzuru kwa Josef Ratzinger, kuonyesha kwamba, katika mwamba ambayo Kristo amejengwa Kanisa lake, pia bado una utendaji wa mtu binafsi katika maamuzi yake kwa manufaa ya kanisa na ofisi ya Papa" Na tena: Haya ni maamuzi ya dhamiri na uchaguzi binafsi wa Ratzinger, alioufanya kwa mujibu wa sheria ya Kanisa ya mwaka 1917."
Kardinali Donald Wuerl, Askofu Mkuu wa Washington, pia ameiambia Redio Vatican kwamba, Kujiuzuru kwa Papa kumezingatia mahitaji ya “Papa katika nyakati hizi za Kisasa ambamo Papa anatakiwa pia kuwa na ratiba nyingi za kusafiri hapa na pale, kwa ajili ya kuimarisha waamini katiak maeneo mengi zaidi duniani. Na hivyo kwa busara na hekima Papa Benedikto XV1, ameona haNa tena nguvu za kufanya hivyo , badala ya kung'ang'ania anaona umefika wakati wa mtu mwingine ambaye anauwezo zaidi kimwili kusonga mbele ratiba muhimu za Kanisa la Ulimwengu.

Pia Kardinali Emmanuel Wamala, Mstaafu Askofu Mkuu wa Kampala Uganda , amesema kuwa, sote tunapaswa kuheshimu maamuzi yake, na kumwombea, kama yeye anavyoahidi kutuombea pia.










All the contents on this site are copyrighted ©.