2013-02-18 15:07:36

Kwaresima ni wakati wa Mapambano- Papa


Jumapili maelfu ya watu alimiminika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, kusali sala ya Malaika wa Bwana pamoja na Baba Mtakatifu Benedikto XV1, katika kukianza kipindi cha Kwaresima.

Papa akihutubia kutokea dirisha la chumba chake cha kujisomea katika jengo la Kipapa, aliwasisitiza waamini katika kipindi hiki cha kwaresima , ambamo Mama Kanisa anaadhimisha Mwaka wa Imani, kwamba ni wakati muafaka wa kugundua upya imani kwa Mungu, kuwa ni kigezo msingi katika maisha yetu na maisha ya kanisa.

Papa aliendelea kwamba , hiii inamanisha ni mapambano ya kiroho, kwa sababu roho wa ibilisi ambaye yu kinyume na utakatifu wetu, daima hutafuta kutuweka nje ya maisha ya Matakatifu ya Kimungu yaliyondaliwa kwa ajili yetu. Hivyo kwa ajili hiyo Kanisa daima katika Jumapili ya kwanza ya Kwaresima, hurejea somo la Injili, la Yesu alivyojaribiwa Jangwani na Ibilisi wakati wa siku 40 za mafungo.

Papa alieleza , Ibilisi ni mwerevu, hatushinikizi moja kwa moja kutenda maovu, lakini kwa hira huyaingilia maisha yetu na vishawishi vya mambo mazuri bandia, yanayoweza kuonekana kama ni muhimu kwa wakati huo na kumbe ni mtengo wa kwenda kinyume na imani kwa Mungu .

Papa amesema, katika muda muhimu wa kutoa maamuzi katika maisha, mtu anapaswa kuwa makini sana , maana ni sawa na kusimama katika njia panda au uchague njia hii au njia ile. Ni kuchagua au kuzifuata nia binafsi, au kuisikiliza sauti ya Mungu.

Papa alieleza na kutolea maombi kwa Mungu akisema , leo hii tunapo tafakari Yesu jangwani, ambako alikwenda kufunga na kusali, na pia anajaribiwa na iIbilisi, pia kwetu unakuwa ni wakati wa kukianza kipindi cha kwaresima, tukiwa tumeungana pamoja , kuomba msaada wa Mungu, utuimarishe katika kupambana na madhaifu yetu.

Papa pia aliutumia muda huo, kutoa shukurani zake za dhati kwa waumini wote kwa sala na faraja walizozionyesha tangu alipotangaza nia yake ya kustaafu Kiti cha Petro, ambacho atakiachia rasmi wiki ijayo tarehe 28 Februari 2013.








All the contents on this site are copyrighted ©.