2013-02-14 13:47:15

Vatican na Serikali ya Italia watia sahihi katika itifaki ya matumizi ya viunga vya mji wa Roma


Serikali ya Italia kupitia Wizara ya Utamaduni na Mambo ya Kale pamoja na Vatican, tarehe 14 Februari 2013 wametiliana sahii Itifaki ya matumizi ya mtaa unaojulikana kama "Passetto di Borgo na ule wa Torrino" kama njia ya ushirikiano wa dhati unaopania kulinda na kuendeleza urithi wa kihistoria, kitamaduni na mambo ya kale.

Lengo ni kuwawezesha watu kutembelea maeneo haya kwa kuzingatia pia mahitaji ya watu wenye ulemavu. Baada ya ukarabati mkubwa, Serikali ya Italia itafungua tena kiunga hiki, ili watu waweze kupata nafasi ya kutembelea Makumbusho ya Kitaifa yaliyoko "Castel Sant'Angelo".

Itifaki hii imetiwa sahihi na Kardinali Giuseppe Bertello, Rais wa utawala wa Mji wa Vatican pamoja na Professa Lorenzo Orhaghi, Waziri wa Utamaduni na Mambo ya Kale nchini Italia na kushuhudiwa na viongozi waandamizi kutoka pande zote mbili.







All the contents on this site are copyrighted ©.