2013-02-09 15:46:55

Tahariri: Vijana katika ulimwengu wa tamaduni nyingi


Kwa Jinsi gani tunaweza kuelewa hisia, fikira,na namna ya kujieleza kwa vijana? Amehoji Padre Federico Lombardi katika tahariri yake ya wiki hii , na kutoa jibu kwamba ni vigumu, kwa sababu ya upeo wa macho ya leo,unazidi kukanganyikiwa na mabadiliko ya haraka sana, mabadiliko ya kiakili, mila, tabia.
Na ndivyo ilivyo , kama alivyosema Papa ,hali hiyo, ni utamaduni ulioenea ulimwenguni kote, kwa lugha nyingi tofauti zinazoonekana katika tabia, sifa na wingi wa maono na mitazamo.

Na hivyo kutokana na ugumu huu, Baraza la Kipapa kwa ajili ya Utamaduni, linaona haja ya kidharura, kutafakari juu tamaduni za vijana.
Jitihada zinazotafutwa ni kukazia utoaji wa majibu sahihi katika maswali msingi na muhimu katika haja za vijana. Ni kutoa majibu ya kueleweka, katika lugha nyepesi na mbinu zenye mikakati ya kuweza kuifikia au kuigusa mioyo na akili za vijana, kama walivyo.
Padre Federiko Lombardi anaendelea kuzitazama haja za vijana, hata katika ulimwengu wa tarakimu(digital) na muziki wa pop au rock, akisema yote hayo yanaweza yasikidhi majibu yetu. Kwa kuwa hhayo haitoshi, kupata jibu sahihi, kunatoa hoja ya kushirikiana na vijana kwa ukaribu zaidi, kuwapenda na kuwa na imani nao kama alivyoeleza Baba Mtakatifu. Ni kushirikianao nao bega ka bega katika uchambuzi wa kulipata jibu linalowafaa na kuwasadikisha kwamba wao ni watu wazima wa kesho.
Na kwamba ndani ya Kanisa, daima kuna waelimishaji wengi wa ajabu na marafiki wa kweli wa Vijana, ambao wanaweza kuwa msaada mkubwa kwa vijana kupata jibu linalofaa linalotafutwa na vijana. Kanisa daima haliwakatishi tamaa au kuwapuuza vijana, badala yake katika nyakati zote hutafuta kutembea na vijana katika maisha yao kwa ajili ya kuipata maana ya kweli ya maisha.








All the contents on this site are copyrighted ©.