2013-02-09 15:33:44

Mkristu wa kweli haogopi vitisho vya kuifia imani


Baba Mtakatifu Benedict XVI, Ijumaa aliendeleza jadi yake ya kila mwaka kutembelea Seminari Kuu ya Jimbo la Roma, katika kuiadhimisha Siku Kuu ya Kiliturujia ya Mama yetu wa Matumaini. Akiwa katika seminari hiyo, alionyesha kufurahia wingi wa vijana wanaofuata njia inayo waelekeza katika maisha ya Upadre, wakimtafuta Bwana wa Kweli wa nyakati hizi zetu.
Hotuba yake kwa wanafunzi, na wafanyakaziwa Seminari hiyo, ililenga katika Barua ya Kwanza ya Mtume Petro sura ya kwanza , mistari 3-5... Ahimidiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kuu tumezaliwa upya kwa matumaini, kupitia njia ya ufufuo wa Yesu Kristo kutoka kwa wafu, na urithi usio haribika, wala kuwa na dosari, wala kufifia, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu......
Papa Benedikto, alitoa tafakari juu ya maandishi hayo akisema, barua hiyo ya kwanza ya Mtume Petro, iliyoelekezwa moja kwa moja katika makanisa ya Asia , kwa namna fulani ni Waraka wa kwanza wa Kipapa ,ulioandikwa na Askofu wa Roma wa Kwanza, unao lizungumzia kanisa zima la Ulimwengu lkatika kila enzi.
Papa Benedikto, aliendelea kueleza na kutetea uhalisi wa uandishi wa waraka huo akisema, ina ufahamu mkubwa wa kikanisa kuhusu mamlaka na utume wa Petro mwenyewe.
Papa pia alitafakari masharti kadhaa muhimu na mandhari ya barua, ikiwa ni pamoja na urithi, wito Mkristu katika furaha ya kweli ya kuwa mteule wa Mungu , mahusiano ya Kikristo –katika furaha yake ya kuwa raia wa Yerusalemu ya Mbinguni , na mamlaka za kiraia na wajibu wake , haki zake na uwajibikaji wake katika kutunza taratibu na mielekeo na tabia yake sahihi katika uraia wa kidunia.
Na kwamba, Petro hazungumzi kama mtu binafsi lakini kama mtu wa kanisa , katika ukuu wa uwajibikaji wake, katika usharika wa kanisa.
Mtume Petro, alifahamu hatari za kifo alizokuwa akikabiliana nazo Roma, lakini hakurudi nyuma , aliendelea kutembea katika njia ya msalaba iliyoonyeshwa na Kristu, na hivyo hata leo hii, anatoa mwaliko kwa watu wa leo, kuipokea imani kwa uthabiti hata kama ni kukabiliana na kifo. Alisema, Hakuna anayeweza kuwa mfuasi wa Msulubiwa bila kukubali pia kuyatolea katika kifo.
Papa alikiambia kikundi cha vijana zaidi ya 190 ambao wako katika majiundo yao ya kutaka kulitumikia Kanisa la ungu . Na kwa Namna ya pekee, Papa alisema uchaguzi wao , ni uchaguzi wa namna yake , kwa maana Bwana ndiye anayemuita kila binadamu. Daima huwa ni mapenzi ya Mungu , kwa ajili ya kuitambua sura ya Kristu na hivyo Ukatoliki daima unakuwa ni zawadi ya Mungu.
Daima tunapaswa kufurahia hili kwa kuwa Mungu ametupatia neema hizi. Uzuri huu wa kutambua ukamilifu wa ukweli wa Mungu na furaha ya upendo wake.








All the contents on this site are copyrighted ©.