Kanisa na nyumba ya Parokia kujengwa nchini Cuba kama kumbu kumbu ya hija ya kichungaji
ya Benedikto XVI nchini Cuba
Serikali ya Cuba imetoa ruhusa kwa Kanisa nchini humo kujenga Kanisa na nyumba ya
Parokia kama sehemu ya kumbu kumbu endelevu ya hija ya kichungaji ya Baba Mtakatifu
Benedikto wa kumi na sita nchini Cuba, mwezi Machi 2012. Hizi pia ni juhudi za Serikali
ya Cuba kutaka kurudisha sehemu ya mali ya Kanisa iliyotaifishwa kwenye miaka ya 1960,
wakati utawala wa Kikomunisti ulipokuwa umepamba moto.
Viongozi wa Kanisa wametoa
shukrani zao za dhati kwa Serikali kutokana na uamuzi hii hatua ambayo itaendeleza
majadiliano na ushirikiano kati ya pande hizi mbili kwa ajili ya mafao na maendeleo
ya wananchi wa Cuba: kiroho na kimwili.