2013-02-05 09:42:23

Papa ateta na Rais Napolitano wa Italia


Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita pamoja na Rais Giorgio Napolitano wa Italia, kabla ya kuhudhuria Tamasha la Muziki, kama sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 84 ya Mkataba wa Laterano, uliotenganisha shughuli za Kanisa na Serikali ya Italia, walifanya mazungumzo ya faragha kwa takribani dakika 20.

Mazungumzo haya yamekuwa ni muhimu sana wakati huu, Rais Napolitano anapojiandaa kung'atuka kutoka madarakani baada ya kuwaongoza wananchi wa Italia katika kipindi cha miaka saba ya shida na changamoto kubwa kutoka ndani na nje ya Italia yenyewe.

Viongozi hawa wawili wanaoheshimiana na kuthaminiana katika utekelezaji wa majukumu yao, wamezungumza kwa kina na mapana kuhusu matukio mbali mbali yanayotarajiwa kufanyika nchini Italia. Wamejadili pia masuala mbali mbali yanayoigusa Jumuiya ya Kimataifa, lakini kwa namna ya pekee, ukosefu wa msingi ya haki na amani huko Mashariki ya Kati na Afrika.







All the contents on this site are copyrighted ©.