Serikali ya Tanzania inapania kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi
Waziri mkuu Mizengo Pinda amesema kila Halmashauri nchini Tanzania ina wajibu wa kuhakikisha
kuwa mipango inayowekwa inalenga kusadia watoto walio katika mazingira hatarishi.
Ametoa kauli hiyo Februari Mosi, 2013 wakati mamia ya wazazi na wanafunzi walioshiriki
uzinduzi wa Mpango Kazi wa Pili wa Taifa wa Watoto walio katika Mazingira Hatarishi
uliofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma. Mpango
Amesema wadau wakuu
katika kutekeleza mpango kazi huo wa miaka mitano (2013 -2017) ambao ni Halmashauri
zote nchini, Serikali Kuu, Bunge, Mahakama, washirika wa maendeleo, asasi zisizo za
kiserikali na madhehebu ya dini wana mchango mkubwa wa kuhakikisha hali za watoto
hao zinabadilika. “Kila Halmashauri itekeleze wajibu inavyotakiwa. Wenyeviti wa Serikali
za Vijiji, Madiwani ni lazima tuhakikishe mipango yetu inalenga kusaidia watoto walio
katika mazingira hatarishi,” alisema.
Waziri Mkuu alisema wadau wengine wakuu
katika kutekeleza mpango kazi huo ni Serikali Kuu ambapo alizitaka Wizara Mtambuka
zinahusika na suala hili zijipange kuhakikisha mpango huo unatekelezwa na kusaidia
kubadilisha maisha ya watoto hao. Alisema Bunge kwa upande wake, ambalo liliwakilishwa
kwenye uzinduzi huo na wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii, litasaidia kuhakikisha
fedha inayopangwa inapatikana kwa wakati na inatumika vizuri.
Akisisitiza kuhusu
jukumu la kulea na kutunza watoto ni la kila mmoja, Waziri Mkuu alisema: ”Watanzania
mmoja mmoja ni lazima tuonyeshe upendo kwa watoto kwa sababu mtoto wa mweinzi ni mtoto
wako. Usimuone mtoto wa mwenzio anafanyiwa ukatili au ana hali mbaya ukasema shauri
yake, huyu si wa kwangu”. Alizitaka pia Wizara ya Mambo ya Ndani na Wizara ya Afya
na Ustawi wa Jamii zikae pamoja na kuwaita wadau wake ili ziweze kujadiliana njia
bora ya kutoa huduma vizuri zaidi kwa jamii wanazozihudumia kwenye mikoa mbalimbali
badala ya kuachia asasi nyingi kuwa zimejirundika katika mikoa michache tu.
Mapema
wakisoma risala yao, watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu walisema tangu mpango
huo uanze mwaka 2007, wamenufaika kwa kupatiwa vifaa vya shule, sare za shule, mablanketi
na ada. Walisema mpango huo umewasaidia kuwafanya wajiamni wawapo shuleni tofauti
na hapo awali ambapo wenzao walikuwa wakiwadhihaki na kuwatenga kwa kukosa sare au
kuwa wachafu wawapo shuleni kwani hawakuwa na nguo za kubadilisha.
Walitumia
fursa hiyo kuomba wanapofaulu, wapatiwe nafasi za bweni ili wawe na uhakika wa kumaliza
shule, wasidaiwe michango mbalimbali shuleni na wakipata nafasi ya kwenda elimu ya
juu, wapatiwe ufadhili na serikali kwa asilimia 100.