Askofu Joseph Effiong Ekuwem ateuliwa kuwa Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Calabar, Nigeria
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, amekubali ombi la Askofu mkuu Joseph Edra
Ukpo wa Jimbo kuu la Calabar, Nigeria la kung'atuka kutoka madarakani na badala yake
amemteua Askofu Joseph Effiong Ekuwem kuwa Askofu mkuu wa Jimbo la Calabar. Kabla
ya uteuzi huu, Askofu mkuu mteule Ekuwem alikuwa ni Askofu wa jimbo la Uyo, Nigeria.