2013-01-30 14:20:19

Zaidi ya watu 50,000 Msumbiji hawana makazi kutokana na mafuriko!


Mvua kubwa inayoendelea kunyeesha Kusini mwa Msumbiji imesababisha maafa makubwa kiasi kwamba, hadi sasa kuna jumla ya watu 50,000 hawana makazi na kuna uwezekano mkubwa kwamba, watu wakaendelea kupoteza maisha na mali zao.

Takwimu zinaonesha kwamba, kuna jumla ya watu 50 wamefariki dunia kutokana na mafuriko. Wataalam wa hali ya hewa wanasema kwamba, mafuriko ya Mwaka 2013 pengine yakawa ni makubwa zaidi kuliko yale yaliyotokea nchini Msumbiji kunako mwaka 2000, yaliyopelekea watu zaidi ya 800 kupoteza maisha. Waathirika wakuu ni wale wanaoishi kwenye kingo za Mto Limpopo, Kusini mwa Jimbo la Gaza.







All the contents on this site are copyrighted ©.