2013-01-29 07:13:08

Moto mkubwa wateketeza bidhaa nyingi Soko kuu Bujumbura


Wafanyabiashara wengi nchini Burundi wamepoteza mali yenye thamani kubwa kutokana na moto uliozuka kwenye soko kuu mjini Bujumbura, Jumapili, tarehe 27 Januari 2013 na kuteketeza mali iliyokuwa imehifadhiwa sokoni humo. Kutona na hasara kubwa iliyopatikana watu wengi nchini Burundi wanahofia kwamba, bei ya bidhaa itaongezeka maradufu na walaji walazimika kulipia hasara hii.

Inasemekana kwamba, kuna watu kadhaa pia wanahofia kwamba, wamepoteza maisha yao, lakini habari hizi bado hazithibitishwa. Kikosi cha zima moto kilifanikiwa kuzimisha moto huu baada ya kazi kubwa ilyowachukua masaa kadhaa. Rais Pierre Nkurunziza aliyekuwa mjini Addis Ababa akihudhuria mkutano wa Wakuu wa Umoja wa Afrika, alilazimika kurejea nchini mwake ili kujionea mwenyewe hali halisi.

Baada ya kurejea nyumbani ameitisha mkutano wa dharura wa Kamati ya Usalama ya taifa ili kuangalia hatua za kuchukua na kwamba, amewaomba Wasamaria wema ndani nan je ya Burundi kuwasaidia watu walioathirika na moto huo.








All the contents on this site are copyrighted ©.