Maafa nchini Malawi! Watu 641 hawana makazi kutokana na mvua kubwa
Zaidi ya familia 641 kutoka Uwambo, Wilaya ya Zomba, Malawi hawana makazi baada ya
nyumba zao kusombwa na mafuriko hivi karibuni kutokana na mvua kubwa inayoendelea
kunyeesha nchini humo. Mvua hii pia imesababisha uharibifu mkubwa wa mazao mashambani
baada ya mafuriko hayo kuharibu pia Bwawa lililokuwa limejengwa ili kudhibiti maji.
Waathirika hawa wanahitaji msaada wa dharura ili kuweza kukabiliana na hali
hii ngumu. Kwa sasa watu wanahitaji: chakula, maji safi na salama, nguo na blanketi
za kujifunika. Licha ya vifo vilivyotokea lakini pia kuwa watu 5,000 ambao wamepoteza
kila kitu kutokana na mafuriko hayo. Serikali ya Malawi inaendelea kujikakamua kutoa
msaada kwa waathirika hao.