2013-01-23 15:43:38

Waamini jifunueni katika baraka za Mungu ili mweze kuwa baraka kwa Wengine- Papa


Baba Mtakatifu Benedikto XV1, akiendelea na Katekesi juu ya sala ya Muumini, Jumatano hii, aliielekea sala ya Nasadikiā€, sala Msingi katika Imani ya Mkristu.
Alisema , katika mwaka huu wa Imani, ninapenda kutoa lafakari mfululizo juu ya sala hii, ambayo tunaikiri. Tangu mwanzo wa Ibada, tunakiri imani yetu kwa Mungu tukisema, Nasadiki katika Mungu, na hivyo ni uthibitisho msingi, na mwepesi katika sifa zake, na ni kujifunua kwenye dunia isiyokuwa na ukomo, katika uhusiano na Bwana na fumbo la wokovu.
Papa aliendelea kusema, Nasadiki kwa Mungu kunamaanisha ni kushikamana Naye, kulipokea Neno lake na kutii kwa furaha ufunuo wake. Kama inavyofundisha Katekismo ya Kanisa Katoliki , Imani ni kitendo cha mtu binafsi , kwa uhuru wake kamili, kutoa jibu linalo kukabiliana na mpango wa Mungu, ambaye amejifunua mwenyewe kwa Binadamu..
Kwa maneno Mengine , tunaweza kusema, kusadiki kwa Mungu hivyo inakuwa pia ni zawadi, kazi na Neema Takatifu na uwajibikaji wa binadamu katika utendaji wa majadiliano na Mungu, ambaye kwa upendo , anaongea na wanadamu kama rafiki. Mungu anaongea na sisi kwamba, katika imani na kwa imani, sisi tunaingia katika ushirika pamoja naye.
Papa alihoji ni wapi tunaweza kumsikia Mungu akizungumza na sisi? Na alitoa jibu kwamba, Kimsingi, ni katika Maandiko Matakatifu, ambamo Neno la Mungu huweza kusikika kwa ajili yetu na kulisha maisha yetu kama marafiki wa Mungu. Maandishi yote ya Biblia , huzungumzia kujifunua kwa Mungu kwa binadamu. Na pia inazungumzia imani na kufundisha imani kupitia simulizi za Kihistoria ambamo Mungu anafanikisha Mpango wake wa Wokovu na kujiweka karibu na binadamu , kupitia watu mbalimbali, waliomsadiki Yeye na kumtumaini Yeye, kwa utimilifu wa ufunuo wa Bwana Yesu Kristu.
Papa ameeleza kwa kurejea Maandiko Mtakatifu mbalimbali ya Biblia, historia ya ufunuo wake na kuja kwake Mwana wake, Yesu Kristo. Tangu kufunuliwa kwa Abrahamu, baba na mfano wa waumini wote (taz. Rum 4:11-12) anayedumishwa na baraka ya Mungu na imani katika ahadi Yake, Abrahamu aliondoka kuelekea asipopajua.
Na Vinyo hivyo kama Abrahamu, sisi pia, twaitwa kuiachia Imani yetu, itengeneze mawazo na utendaji wetu kwa mujibu wa Neno la Kuokoa la Mungu hata kama tunakuwa kinyume na mawazo na njia za utendaji za dunia hii. Kwa macho ya imani, sisi tunatambua uwepo wa Mungu na ahadi yake ya uzima wa milele, zaidi ya hali halisi ya uwepo wa usasa . Ni kujifunua wenyewe katika Baraka za Mungu , ambamo tunaweza pia kuwa baraka kwa wengine.
Baada ya Katekesi , akisalimia katia lungha mbalimbali, Papa aliwa kumbuka wahanga wa hali mbaya ya hewa iliyokumba mji wa Jarkata ambako mamelfu ya watu wanateswa na uharibifu wa majengo na mali uliofanywa na maporomoko ya aridhi.
Alisema katika maafa haya asilia, niko karibu na wote wanaoteswa na hali hiyo , na aliwahakikishia ukaribu wake kupitia sala na akahimiza watu wote kuwa na mshikamano wa karibu na wahanga hao , ili wasikose mahitaji yao muhimu.








All the contents on this site are copyrighted ©.