Waachieni Mapadre mliowateka, ili wamtumikie Mungu na Jirani zao!
Baraza la Maaskofu Katoliki DRC limerudia tena ujumbe wake, kwa kuwaomba watu ambao
waliwateka nyara Mapadre watatu wa Shirika la Assumption, Mwezi Oktoba 2012 kuwaachia
mara moja, ili waweze kuendeleza huduma kwa waamini wao kiroho na kimwili.
Maaskofu
wanasema, Mapadre hawa waliotekwa hawana sababu ya kuendelea kuteseka katika mazingira
hayo. Ni nafasi kwa wateka nyara kutubu na kuongoka, kwa kuwaachia ili waendelee kutekeleza
wajibu wao. Mapadre waliotekwa tangu mwezi Oktoba, 2012 ni Jean Pierre Ndulani, Anselme
Wasikundi pamoja na Padre Edmond Bamutate.
Mapadri hawa walitekwa nyara hapo
tarehe 19 Oktoba 2012 walipokuwa kwenye Parokia ya Notre Dame des Pauvres iliyoko
Mbau, Jimbo Katoliki la Butembo, DRC. Tangu wakati huo, hakuna taarifa juu ya Mapadre
hawa.