Kardinali Ravasi kuongoza Mafungo ya kiroho ya Papa na Curia
Kardinali Gianfranco Ravasi, Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili a Utamaduni , atakuwa
Mhubiri wa mafungo ya Papa ya wiki moja tangu tarehe 17 hadi 23 Februari, kwa ajili
ya kuikianza kipindi cha kwaresima kwa mwaka huu 2013. Mahubiri yake yataongozwa
na Mada: Sura ya Mungu ni Sura ya Muumini katika Zaburi ” Ars Orandi Ars Credendi”.
Kardinali Ravasi ametaja sababu ya kuchagua aya hiyo ya zaburi akisema, ni kwa
kuwa, katika sala, Mungu na Binadamu hukutana na kujadiliana. Na kwake yeye anaiona
ni heshima kubwa kuchaguliwa na Papa kuwa mhubiri wake katika kukianza kipindi hiki
muhimu cha Kanisa. Na hivyo ni katika mwamko huo wa kiroho, pia kibindamu linamsisimua
kuzama katika kina cha tafakari kwa ajili ya kipindi hiki cha Kwaresima. Na pia kwa
upande mwingine haya ni majadilaino ya ndani ya watu wanaofanyakazi karibu na Papa.