Baba Mtakatifu amemteua Padre Dario Edoardo Vigano,mwenye umri wa miaka 51, kuwa Mkurugenzi
Mpya wa Kituo cha Runinga cha Vatican. Padre Dario, ni Padre wa Jimbo Kuu la Milan
na anachukua nafasi inayoachwa wazi na Mkurugenzi wa sasa Padre Federico Lombardi
mwenye umri wa miaka 71, anayestaafu kwa mujibu wa umri. Aidha Baba Mtakatifu
amemteua Mwana Habari Mlei, Dk Angelo Scelzo, kuwa Naibu Mkurugenzi wa Ofisi ya Habari
ya Jimbo la Papa. Hadi kuteuliwa kwake, alikuwa Katibu mwandamizi katika Baraza la
Kipapa kwa ajili ya Mawasiliano Jamii. Na pia Papa amemteua Mons. Gerardo Antonazzo
, Padre wa Jimbo la Ugento – Santa Maria di Leuca, kuwa Askofu wa Jimbo la Sora-
Aquino Pontecorvo, Italia. Hadi kuteuliwa kwake alikuwa ni Vika Mkuu w Jimbo hilo.