2013-01-21 09:10:34

Juma la Kuombea Umoja wa Wakristo siku ya Nne: kutembea kama watoto wa dunia


Katika siku hii ya nne wazo letu kuu ni kutembea kama watoto wa dunia. Kama tunatembea katika unyenyekevu na Mungu tutahitaji kujitambua daima kuwa ni viumbe na sehemu ya viumbe vya Mungu na hivyo wapokeaji wazawadi za Mungu. RealAudioMP3
Tuepe Vitu vinavyotutenganisha na ufahamu kwamba mahusiano na mazingira ni sehemu muhimu ya safari yetu, ya maisha yetu na mahusiano yetu na Mungu na muumbaji, kwa kuwa yote tuliyonayo tumepewa naye na hivyo si vyetu kuvifanyia tutakavyo.
Simulizi la kikristo ni la Wokovu kwa viumbe vyote. Ni simulizi linalojihusu - uumbaji Imani yetu ni kwamba katika Yesu, Mungu anatwa mwili katika historia yaani katika muda na wakati unaojulikana ni imani ambayo ni kitovu au mhimili ambamo wakristu wote wanakusanyika na kukutana.
Ni imani katika umwilisho ambayo inabeba maana na ufahamu mzima wa umuhimu wa uumbaji wa miili, chakula, dunia, maji, na kila kinacholisha maisha yetu kama watu tunaoishi katika sayari hii. Yesu ni sehemu kamilifu ya ulimwengu huu. Inaweza kuwa inatisha kidogo kusikia jinsi Yesu anavyoponya kwa kutumia udongo na mavumbi, lakini ni kweli katika maana ya ulimwengu huu ulioumbwa kama sehemu ya tendo lake la kuumba na kuleta maisha mapya.
Katikati ya ulimwengu, dunia daima hufanyiwa kazi na watu maskini, ambao mara nyingi huwa hawashiriki katika matunda ya matokeo ya kazi, hizi ndizo onjeleo za maskini wengi na mifano tunaijua sana katika mazingira yetu, kama kule uhindini, kwa Wadalit. Kwa upande mwingine ni wadalit wanaotunza wanaotunza mazingira kama hekima ya kuilima ardhi inavyoonyeshwa katika kazi.
Kuitunza dunia ni pamoja na kujiuliza swali la msingi ni kwa jinsi gani wanadamu wanaweza kuishi wakihusiana vizuri na viumbe wengine wakiheshimu hulka yao kama watu - Dunia, utajiri na umiliki wake visiwe chanzo cha matatizo ya kiuchumi na chemchem ya dharau kwa watu. Wakristo lazima wajiulize hili kwa pamoja.
Hatari ya kuitumia dunia vibaya na agano la kuitunza dunia linaongelewa katika kitabu cha Walawi kuhusiana na mwaka wa Jubilee: ardhi na matunda yake havijatolewa kwa ajili kumnyanyasa mwingine, bali ni kwa manufaa ya wanadamu wote. Hii si tunu tu ya kidini bali inagusa pia uchumi na biashara - kwani inahusu pia ni kwa namna gani ardhi inamilikiwa, inauzwa na kununuliwa.

SALA
Mungu wa maisha tunakushukuru kwa kutupa dunia na wale wote wanoitunza ili itupe chakula. Tunaomba Roho mtakatifu mpaji wa uzima atusaidie kutambua kwamba sisi ni sehemu ya uumbaji wako na mahusiano kati ya viumbe vya dunia. Tunaomba tujifunze kuitunza dunia na kusikiliza kilio cha chake. Tunaomba tutembee pamoja na Kristu ili kuponya madonda yote tuliyosababisha kwa dunia na kushiriki kwa haki matunda ya dunia. Mungu wa upendo tuongoze katika njia ya haki na amani. Amina


MASWALI
Masomo ya leo yanamualika Mkristo katika kuwajibika kwa pamoja kwa kina kuhusiana na kuutunza ulimwengu. Je ni wapi tunatekeleza kimatendo roho ya Jubilee kama wakristu kwa pamoja?
Ni wapi kama jumuia tunavikosea vitu haki hivyo kwamba tunavitumia kama nyenzo za kubeza na kuudhalilisha ulimwengu? Ni wapi tunaweza kufanya kazi, kujifunza na kufundisha kwa pamoja juu ya kuheshimu uumbaji na viumbe vya ulimwengu?
Tafakari hii imeandaliwa na Padre Emmanuel Nyaumba.








All the contents on this site are copyrighted ©.