Juma la Kuombea Umoja wa Wakristo siku ya tatu: kutembea kuelekea uhuru
Katika siku hii ya tatu ya kuombea Umoja wa Kanisa, wazo letu kuu ni kutembea kuelekea
uhuru. Kutembea kinyenyekevu na Mungu maana yake kuwa daima tayari kupokea uhuru ambao
Mungu anaufungua kwa wanadamu wote. Tukiwa na wazo
hili tunasherehekea fumbo la kujikomboa kiuhuru yaani kutafuta uhuru wa kweli. Ni
fumbo ambalo linatukia hata katika sehemu ambamo manyanyaso, chuki, ubaya na umaskini
uliotopea vinaonekana kuwa ni mzigo mkubwa. Kukataa kabisa kukubali amri na hali
za onevu kama zile zilizotolewa na Farao kwa wakunga waliowahudumia watumwa wa kiyahudi
inaweza kuonekana kama ni jambo dogo lakini mara nyingi haya ni matendo ambayo yanatukia
katika maeneo tunayoishi kila siku. Hivyo tunasherehekea kupewa uhuru; kwa heshima,
kiutu, na kushiriki kikamilifu katika yale yaliyo mema kama yale tunayofanya katika
jumuia zetu au tunayojitendea wenyewe. Safari hii ya maisha ya pamoja kuelekea maisha
ya kweli ni zawadi ya enjili ya matumaini kwa watu wote. Zawadi hii imejikita katika
tofauti zetu katika mfumo wa kutofanana ulimwenguni. Hatua kwa hatua tutaweza kufikia
uhuru kutokana na kubaguliwa na kuchukiana. Ujumbe huu unajieleza vizuri zadi
katika simulizi la Yesu na mwanamke msamaria. Mwanamke huyu anatafuta kwanza kujua
chanzo cha kubaguliwa na chuki inayomzunguka pia kutafuta njia za kutibu hali hii
na mizigo aliyo nayo maishani mwake. Wajibu huu alionao ni mwanzo wa kuongea kwetu
na Yesu. Yesu mwenyewe anaungana naye kuongea naye katika mahitaji yake, ya kiu
yake, yanayohitaji msaada, anamfafanulia hali ya kijamii ya kubezwa aliyo nayo ambayo
inafanya msaada huu uwe ni shida yake. Pole pole njia ya uhuru inafunguliwa kwa huyu
mwanamke kwa vile hali ya maisha yake inatazamwa kwa muelekeo wa Neno la Mungu yaani
la Yesu mwenyewe. Mwisho, mang'amuzi haya yanayarudisha maongezi yao kwenye hatu
ambayo inawatenganisha wasamaria na Waisrael yaani mahali pa kuabudia - pale pa kuabudia
ni mahali zaidi ya mahali au sehemu inayoonekana. Kuabudu katika roho na kweli ndiko
kunahitajika na hapa ndipo tunapojifunza kuwa huru kutokana na yote ambayo yanaturudisha
nyuma maishani; kama Wakristo tunaotafuta umoja na kama watu ambao tunapaswa kuzipa
changamoto tamaduni zisizokuwa na haki na usawa ndani yake; zinazotufanya watumwa
bado na tuliofichika kwa wengine. Uhuru wetu ndani ya Kristo una sifa ya maisha
mapya ndani ya Kristo, maisha ya roho mtakatifu maisha ambayo yanatuwezesha kusimama
mbele ya utukufu wa Mungu, kwa nyuso za wazi. Ni katika mwanga huu wa utukufu tunajifunza
kujiona sisi kwa sisi kikweli kama tunavyokua katika kuelekea ukomavu au ukamilifu
wa umoja wa Kanisa.
SALA: Ee Mungu unayetupa uhuru asante sana kwa imani
iliyojaa ujasiri na matumaini kwa ajili ya wale wanaopambana kuleta heshima na ukamilifu
wa maisha. Tunajua kwamba unawainua wale walioanguka na kuwapa uhuru wale waliofungwa.
Mwana wako Yesu Kristo anatembea nasi kutuonyesha njia halisi na sahihi ya uhuru.
Tunaomba tutambue daima kile ambacho kimetolewa kwetu. Na tuimarishwe tuweze kuyashinda
yaleyanayotufanya watumwa ndani yetu. Mtume Roho wako mtakatifu ili atupe uhuru, ili
tukiwa na sauti zilizoungana kwa pamoja tunaweza kutangaza upendo wako kwa ulimwengu.
Mungu wa uzima utuongoze katika haki na amani. Amina. MASWALI: Je, kuna nyakati
katika jumuia zetu za kikristu, ambapo maamuzi mbele na hukumu ya dunia: kuhusiana
na rangi, madaraja, jinsia, utaifa, elimu, yanatuzuia kuona barabara mwanga wa utukufu
wa Mungu? Je, ni njia gani ndogo na za kimatendo tunaweza kuzichukua, kama wakristu
pamoja, kuleta uhuru wa wana wa Mungu (War 8:21) kwa ajili ya makanisa na jamii kwa
mapana?