Askofu Mathieu Madge Lebouakehan ateuliwa kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Mouila,
Gabon
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, amekubali ombi la kung'atuka kutoka madarakani
lililowasilishwa kwake kutoka kwa Askofu Dominique Bonnet wa Jimbo Katoliki la Mouila,
Gabon. Amemteua Askofu Mathieu Madega Lebouakehan kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki
Mouila kwa kumhamisha kutoka Jimbo Katoliki la Port-Gentil, Gabon.
Askofu
Mathieu Lebouakehan ataendelea kuwa ni Msimamizi wa Kitume wa Jimbo Katoliki la Port-Gentil,
huko Gabon.