Tafakari ya Neno la Mungu: Siku ya kwanza ya kuombea Umoja wa Wakristo
Juma la Kuombea Umoja wa Wakristo kwa Mwaka 2013 linaoongozwa na kauli mbiu ”Kile
ambacho Bwana anataka kutoka kwetu” sehemu ya ujumbe wa Nabii Mika 6:6-8. Kwa hakika
Bwana anawaalika waja wake kutenda hakli, kupenda rehema na kutembea katika fadhila
ya unyenyekevu. Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, anawaalika Wakristo
wote kuwa wadumifu katika kuombea umoja wa Wakristo, wakiongozwa na Roho Mtakatifu,
ili kwa pamoja waweze kuungama kwamba Yesu Kristo ni Mkombozi wa ulimwengu, wakishikamana
ili kukabiliana na changamoto zinazoendelea kuibuka katika ulimwengu wa utandawazi
na maendeleo ya sayansi na teknolojia. Tunalianza wiki la sala kuombea umoja wa
Wakristo Mada inayotuongoza wiki nzima ni kutembea na Mungu katika mazingira yote.
Katika siku hii ya kwanza wazo letu kuu ni kuongea na Mungu tukitembea katika njia
ya imani
Kuwa wanyenyekevu kwa Mungu maana yake kutembea kama mtu anayeongea
na mtu mwingine au na Mungu mwenyewe, daima makini kwa kile tunachokisikia. Tunaanza
wiki la sala kwa ajili ya kuombea umoja wa kanisa tukiwa na mantiki ya kushirikishana
Neno la Mungu,kusoma Biblia ambayo ni mhimili na kifungamanisho cha mazungumzo na
umoja wa kiekumene. Wakati huu tunapata fursa ya kufungua nafsi zetu kwa ajili
ya kujifunza kutoka kwa wengine, kushirikiana katika kile tulicho nacho kwa pamoja
bila kuacha kusikiliza kile ambacho tunatofautiana. Kwa njia hii tunapata kuelewana
na kuendelea mbele katika kile ambacho Mungu anatutaka tufanye. Tunatenda haki na
ukarimu kwa kukaa pamoja kuongea na kusali. Umaskini wa kutengwa unaondolewa kwa namna
hii. Neno la Mungu siku ya leo linatuonyesha kuwa Mungu hana kiburi au ubinafsi
katika kutenda kwake yaani hajijengea jina mwenyewe kama watu wa mnara wa Babeli.
Roho mtakatifu wa Mungu ni utajiri unatuunganisha wanadamu wote tusiwe pweke. Roho
huyu anatufundisha sanaa ya kuwasikiliza wengine, kuwajengea jina wengine. Simulizi
tulilolisikia linaeleza ni kwa jinsi gani tunaweza kushikamana kama msingi wa kujitangaza
mwenyewe. Kwa njia ya pentekoste, yaani kumiminiwa Roho Mtakatifu na kupitia nguvu
ya ufufuo wa Yesu maelewano yanawezekana licha ya tofauti zetu. Sisi tumealikwa kushiriki
kusikiliza zawadi ya hotuba inayotuelekeza kwa Bwana, na kuelekea uhuru. Tumeitwa
kutembea katika Roho. Tunasali pamoja kwa sababu tunahitaji kwenda pamoja katika
hali inayojitokeza ya kupoteza matumaini na kukata tamaa. Ni mawasiliano ambayo yanajikita
katika mantiki ya kwenda kwa pamoja lakini pia katika muktadha wa kupoteza matumaini
na kukata tamaa. Kama makanisa yanayoishi katika hali ya utengano na jamii iliyomegwa
kwa chuki na hofu ya mtu mwingine. Tunaweza kujitambua katika hali hii. Ni hapa
hasa ambapo Yesu anachagua kuungana nasi katika mazungumzo yetu kama alivyofanya
kwa wafuasi wa Emmaus. Yeye hatwai hali ya anayeamuru au kufundisha bali kutembea
kandokando ya mfuasi. Ni hamu yake kuwa sehemu ya mazungumzo yetu na jibu letu la
kumtaka akae nasi na kuongea zaidi nasi ili atuwezeshe kumuona yeye aliye Bwana wa
ufufuko. Wakristo wote wanajua kitu fulani juu ya kukutana na Yesu na nguvu ya
neno lake linalowaka ndani yetu. Neno hili ambalo ni matunda ya maisha ya ufufuko
linatuita kuungana na Kristo kwa ndani zaidi. Mazungumzo ya daima kati yetu na Yesu
- hata wakati tunapoteza njia yanatusaidia sana kutuunganisha na kutuweka pamoja.
SALA
Ee
Bwana Yesu Kristo tunakiri kabisa kwamba sisi ni watu wako tunakushukuru kwa kutualika
kuongea nawe kwa upendo. Ifungue mioyo yetu iweze kushiriki kikamilifu katika sala
yako kwa Baba yako ili tuwe kitu kimoja katika safari yetu kuja kwako. Tuwezeshe kukaa
karibu daima. Tupe ujasiri wa kushuhudia ukweli pamoja. Tunaomba sala zetu ziwakumbatie
wale wanaoomba na kuudumisha umoja. Mtume Roho wako mtakatifu atutie nguvu ya kupambana
na hali ambayo inadharau heshima na huruma ndani ya jamii, mataifa na ulimwengu. Wewe
uliye wa haki tuongoze katika njia ya haki na amani. Amina.
MASWALI:
1.
Ni wapi tunaongea kikweli katikati ya tofauti zinazotutenganisha? 2. Je, mazungumzo
yetu yanalenga mipango yetu binafsi au maisha yanayoleta matumaini? 3. Ni watu
gani tunaongea nao na tunawataka tuongee nao? Kwanini? Tukiwa na wazo hili tunasherehekea
fumbo la kujikomboa kiuhuru, yaani kutafuta uhuru, ambalo linatukia hata katika sehemu
ambamo nyanyaso, chuki na umaskini uliotopea vinaonekana kuwa ni mzigo mkubwa? Imeandaliwa
na Padre Emmanuel Nyaumba.