Watoto wana haki ya kuonja upendo kutoka kwa mama na baba zao!
Askofu mkuu Jean Laffitte, Katibu mkuu wa Baraza la Kipapa la Familia, ametuma ujumbe
wa matashi mema na mshikamano wa dhati kwa watu wote watakaoshiriki katika maandamano
dhidi ya kupinga sheria ya ndoa za watu wa jinsia moja, mjini Paris, Ufaransa, jumapili,
tarehe 13 Januari 2013, kwa kusema kwamba, watoto wana haki ya kupata upendo kutoka
kwa baba na mama zao.
Askofu mkuu Laffitte katika mahojiano kwa njia ya simu
na Shirika la Habari la Zenit, ameshutumu muswada wa sheria ya ndoa za watu wa jinsia
moja kwa kusema kwamba, watu wenye mapenzi mema wana haki ya kupinga sheria ambazo
zinakwenda kinyume cha mafao ya wengi, utu na heshima ya binadamu.
Katika kampeni
yake kuwania nafasi ya Urais nchini Ufaransa, Rais Francois Hollande aliahidi kwamba,
ikiwa kama angeshinda uchaguzi mkuu nchini Ufaransa, angetunga sheria inayoruhusu
ndoa za watu wa jinsia moja. Muswada huu wa sheria unaanza kujadiliwa nap engine,
ukapita na kuanza kutumika kama sheria, baada ya kupitishwa, mwishoni mwa Mwezi Juni,
2013.
Askofu mkuu Jean Laffitte anawapongeza na kuwashukuru watu wote waliosimama
kidete kupinga mmong’onyoko wa maadili; kwa kusimamia mafao ya wengi, kwani kwa asili
ndoa ni kati ya bwana na bibi na wala si kinyume chake. Hii ndiyo taasisi ya kweli
ambamo motto anaweza kuonja upendo wa kweli kutoka kwa baba na mama yake!