Zaidi ya watu 150 wamekwisha poteza maisha katika mapigano ya kikabila nchini Kenya
Chama cha Msalama Mwekundu Kimataifa nchini Kenya, katika taarifa yake kwa vyombo
vya habari kinasema kwamba, kuna watu kumi wamefariki dunia baada mapigano ya kikabila
yaliyotokea kwenye Wilaya ya Mto Tana, usiku wa kuamkia Alhamisi, tarehe 10 Januari
2013.
Kuna idadi kubwa ya watu waliojeruhiwa katika mapigano hayo ambayo tangu
mwei Agosti 2012 yamekwisha pelekea watu zaidi 150 kupoteza maisha. Mapigano ya kikabila
kati ya kabila la Orma na Pokomo yanatokana na kugombania ardhi kwa ajili ya kilimo
na kulishia mifugo. Baadhi ya wachungu wa mambo ya kisiasa wanasema pengine kuna mkono
wa wanasiasa wakati huu Kenya inapojiandaa kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa
kufanyika hapo tarehe 4 Machi 2013.
Hivi karibuni, Kardinali John Njue, Rais
wa Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya aliitaka Serikali kufanya uchunguzi wa kina,
ili kubainisha sababu za chokochoko za kikabila zinazopelekea watu wasiokuwa na hatia
kupoteza maisha yao, ili kujenga misingi ya haki, amani na mshikamano wa kitaifa.