Rais John Mahama wa Ghana aliyeshinda uchaguzi mkuu uliofanyika nchini humo hivi karibuni
kwa asilimia 50.7 ya kura zote zilizopigwa, Jumanne, tarehe 8 Januari 2013 ameapishwa
rasmi kushika madaraka ya kuwaongoza wananchi wa Ghana kwa kipindi kingine cha miaka
mitano. Matokeo ya uchaguzi yalipingwa vikali na Bwana John Kufour wa Chama cha Upinzani
cha N.P.P.
Katika sherehe hizi, Bwana John Kufour alihudhuria pia. Itakumbukwa
kwamba, mara baada ya kifo cha Rais John Atta Mills, Bunge la Ghana lilimpitisha Bwana
John Mahama kuongoza Ghana katika kipindi cha mpito.