Ujenzi wa Barabara Kati ya Tabora na Singida wapamba moto!
Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika sherehe
za uzinduzi wa ujenzi wa miradi ya barabara na daraja katika mkoa wa Tabora kuanzia
tarehe 7 Januari 2013. Pamoja na shughuli nyingine, Jumatatu tarehe 7 Januari 2013
akiwa mkoani humo, Mhe. Rais kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya uzinduzi wa ujenzi
wa Daraja la Mbutu liloko Wilayani Igunga.
Jumanne tarehe 8 Januari 2013,
Rais ataweka jiwe la msingi la uzinduzi wa ujenzi kwa lami wa barabara i)
Nzega – Puge, ii) Puge – Tabora, iii) Tabora –
Ndono na iv) Tabora - Nyahua
Siku ya Jumatano ya tarehe
9 Januari 2013, Rais ataweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya Ndono hadi Urambo.
Uzinduzi wa miradi hii ni sehemu ya utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuhakikisha
kuwa makao makuu ya mikoa yote yanaunganishwa kwa barabara za lami. Miradi hii ni
mafanikio makubwa katika sekta ya usafirishaji na itatoa chachu kubwa kwa uchumi wa
mkoa wa Tabora na Taifa kwa ujumla. Aidha, miradi hii itasaidia sana katika kuimarisha
Usafiri wa barabara kati ya Tabora na mikoa ya Kigoma, Shinyanga, Singida na Dodoma.