2013-01-03 11:14:36

Vijana wa Taizè waanza hija ya kiroho Istanbul ili kushiriki Siku kuu ya Tokeo la Bwana, hapo tarehe 6 Januari 2013


Baada ya Vijana wa Kiekumene wa Taizè kuhitimisha mkutano wa thelarhini na tano wa sala mjini Roma, hapo tarehe 2 Januari 2013; tarehe 3 Januari 2013 wameanza hija ya kiekumene, ili kumtembelea Patriaki Bartolomeo wa kwanza wa Kanisa la Kiorthodox la Costantinopoli inayowapatia fursa ya kushiriki pia katika Maadhimisho ya Siku kuu ya Tokeo la Bwana, yaani Epifania hapo tarehe 6 Januari 2013 nchini Uturuki. Hiki ni kikundi cha vijana mia moja kutoka sehemu mbali mbali za dunia wanaokwenda huko ili kusali pamoja na Waamini wa Kanisa la Kiorthodox.

Kwa mara ya kwanza viongozi wa Jumuiya ya Taizè walianza kuwasiliana na viongozi wa Kanisa la Kiorthodox la Costantinopoli mwishoni mwa mwaka 1960 na mwezi Februari 1962 Fra Roger alimtembelea na kusali pamoja na Patriaki Atenagora wa Istanbul. Tangu wakati huo, viongozi mbali mbali wamekuwa wakiwatembelea viongozi wa Kanisa la Kiorthodox ili kuimarisha majadiliano ya kiekumene.

Kunako Mwaka 2005 Fra Roger na Fra Alois walimtembelea Patriaki Bartolomeo na kuoneshwa kuvutwa sana na mikutano ya sala ya vijana inayoendeshwa na Jumuiya ya Taizè, kielelezo makini cha jitihada za kutaka kujenga na kudumisha majadiliano ya kiekumene. Baadhi ya familia za Kikristo mjini Istanbul zimejitolea kutoa hifadhi kwa vijana hao wakati huu wanaposhiriki pamoja nao Maadhimisho ya Siku kuu ya Tokeo la Bwana.







All the contents on this site are copyrighted ©.