Jubilee ya miaka 150 ya kifo cha Mtumishi wa Mungu Pauline Jaricot na miaka 50 ya
utambuzi wa fadhila za kishujaa
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, amemteua Kardinali Paul Poupard, Rais mstaafu
wa Baraza la Kipapa la Utamaduni kuwa mwakilishi wake katika Sherehe za kuhitimisha
Maadhimisho ya Jubilee ya Miaka 150 tangu alipofariki dunia Mtumishi wa Mungu Pauline
Jaricot na miaka 50 tangu Kanisa lilipotambua fadhila za kishujaa; maadhimisho ambayo
yatafanyika hapo tarehe 9 Januari 2013, mjini Lione, nchini Ufaransa.
Kardinali
Paul Poupard ataongozana na Monsinyo Francois Duthel, Msimamizi mkuu wa mchakato wa
kumtangaza Mtumishi wa Mungu Pauline Jaricot kuwa Mwenyeheri pamoja na Mheshimiwa
Padre Daniel Carnot, ambaye aliwahi kuwa ni Mkuu wa Shirika la Kimissionari Barani
Afrika.