2012-12-29 15:30:40

Tahariri ya wiki ya Padre Fedrico Lombardi-


Ujumbe kwa ajili ya Siku ya Dunia ya Amani 2013, uliotolewa na Baba Mtakatifu Benedikto XV1, uliochapishwa hivi karibuni, umetazama kwa kina zaidi mandhari na masuala ya kijamii, katika mahusiano na misingi ya ujenzi wa amani, miongoni mwa jamii. Na ndivyo ilivyokuwa katika ujumbe wa Papa kwa ajili ya adhimisho la Siku kuu ya Noeli, ambamo amelenga moja kwa moja, migogoro inayoendelea, kuanzia hali ya kutisha Syria, ambako kuna ghasia zinazo endelea kumwaga damu ya watu bila ukomo. Na pia katika ujumbe huo, Papa alitoa pongezi na matashi mema kwa viongozi wapya wa Jamhuri ya Watu wa China, katika mtazamo wa majukumu yao mapya , kwenye kuihudumia taifa la China.
Ujumbe huo ulionyesha tumaini kwmaba, pengine hatua hii ya mabadiliko ya viongozi, itakuwa ni hatua mpya katika matumaini ya kuwa na ushirikiano na kanisa katoliki , lakini ukweli wake utajifuanua kawenye hali halisi za utendaji na utambuzi wa matarajio na nia za Papa na Kanisa, kutembea pamoja katika njia ya ubinadamu. Pia ni juu ya Idadi kubwa ya watu wa China ambao ni sawa na moja ya tano ya watu wote duniani,kujiunga katiak mizania hii ya dunia ya ubinadamu.
Na pia kwa ajili ya uhuru wa kidini kwa watu hao kama hitaji muhimu katika ujenzi wa jamii yenye mshikamano na ushirikiano kama Mapapa walivyohimiza kwa mfululizo bila kuchoka, kwamba dini haipaswi kuchukuliwa kama uvujaji wa sheria au uhalifu, au kama sababu ya kuwatenganisha watu au kuingiliwa nje, lakini kama vikosi chanya vya kiroho , vilivyo tayari kuchangia kwa manufaa ya wote.
Kwa roho hii ya umoja na ushirikiano, Jimbo la Papa, daima huijali jamii Katoliki nchini China, kama ambavyo daima limekuwa wazi na nia hii katika ujumbe wote uanopelekwa China na Mapapa wote.
Katika tahariri hii , Padre Federico Lombardi anahoji, iwapo kutakuwa na matumaini hayo katika Mwaka mpya .
Na ameyaweka matumaini hayo kwa Mfalme wa Amani, aliye kuja duniani kwa ajili ya watu wote, wanaoishi katika mataifa madogo na makubwa. "Kama twaitafuta amani , wadogo hawapaswi kuwa na hofu dhidi ya wakubwa. La sivyo, ni wazi kutakuwa na woga".
Na kwamba Papa alitoa Salaam hizi za matashi mema ya amani katika lugha 65,ambazo zilitakiwa kutamkwa katika maelfu ya lugha zote ulimwengu, kwa sababu sisi sote ni familia moja ya binadamu na tuna Baba mmoja.








All the contents on this site are copyrighted ©.