2012-12-28 12:17:53

Wanyama watunzwe, lakini binadamu apewe kipaumbele cha kwanza!


Rais Jacob Zuma wa Afrika ya Kusini anawataka wananchi wa Afrika ya Kusini kudumisha utu na heshima ya binadamu ndani ya familia badala ya kutumia nguvu na rasilimali nyingi kwa ajili ya kujenga urafiki na mbwa, kwamba, kimsingi huu si utamaduni wa mwafrika. Bara la Afrika lina mila na tamaduni njema ambazo zinapaswa kupewa kipaumbele cha pekee kuliko kuiga mambo hata yale ambayo hayana maana sana kwa maisha ya Watu wa Afrika.

Maneno haya ya Rais Zuma yameibua mjadala mzito miongoni mwa wanaharakati na watetezi wa haki za wanyama waliojitokeza katika mitandao ya kijamii kupinga msimamo wa Rais Zuma. Kuna mamillioni ya watu ambao wanakabiliwa na baa la umaskini nchini Afrika ya Kusini, kumbe, kuna mambo yanayopaswa kupewa kipaumbele cha kwanza kwa nchi.

Watu wajifunze kuheshimu na kuthamini utu wa mwanadamu, kwani pale mtu anapohamisha upendo wake kutoka kwa mwanadamu na kuelekeza kwa mnyama, kuna kasoro kubwa anasema Rais Zuma. Wanyama watunzwe, lakini mwanadamu apewe kipaumbele cha kwanza, ndio ujumbe ambao Rais Jaco Zuma alitaka kuufikisha kwa wananchi wa Afrika ya Kusini.







All the contents on this site are copyrighted ©.