Nia ya Papa, kwa sala zake za kawaida, katika Januari, ili kwamba katika mwaka huu
wa Imani Wakristu waweze kuzamisha utambuzi katika Fumbo la wokovu wa Kristu na
utoaji wa ushuhuda kwa furaha, kama zawadi ya imani ndani mwao. Na sala za Papa
kwa ajili ya Misioni, inalenga zaidi ili kwamba, Jumuiya ya Wakristu Mashariki ya
Kati ambao mara nyingi hukumbana na kubaguliwa, waweze kupokea toka kwa Roho Mtakatifu,
nguvu za imani na uvumilivu.