2012-12-26 15:11:12

Papa atafakari maisha ya mfia dini wa kwanza Mtakatifu Stefano


Maadhimisho ya Siku Kuu ya Mtakatifu Stephano ni wito katika kubadili maisha yetu.
Jumatano hii, ambamo Mama Kanisa ameadhimisha Siku Kuu ya Makatifu Stefano, Baba Mtakatifu Benedikto XV1, hakutoa Katekesi yake kwa mahujaji na wageni,akiwa ndani ya ukumbi kama ilivyo kawaida yake kwa siku ya Jumatano. Lakini alijitokeza dirishani kwa nia ya kusali sala ya Malaika wa Bwana, pamoja na wote waliokuwa wamekusanyika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtaktifu Petro.
Na aliutumia muda huo mfupi, kwa mara ingine kutoa salaam zake za matashi mema kwa siku Kuu ya Noel, hutuba fupi ambayo aliiangalisha katika siku kuu ya Kiliturujia ya Mtakaifu Stefano,
Katika hotuba hiyo alisema, katika kuiadhimisha Siku Kuu ya Mtakatifu Stefano, tunaalikwa kuitazama sana sura ya Mwana wa Mungu , ambamo kilele cha furaha ya Noel, kinatuongoza kulitafakari fumbo la Umwilisho wake.
Na kwa ubatizo na Kipaimara , na kwa thamani ya zawadi ya imani inayolishwa na Sakramenti za Kansia , na hasa Ekaristi Takatifu , tunajawa na imani kwa Yesu Kristu kwamba, tumefungamana nae na anaendelea kutaka kubaki ndani mwetu, ili kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, tuiendeleze kazi yake ya kuufikisha ujumbe wa wokovu kwa watu wote, huku akituongoza katika ukamilifu.
Hotuba ya Papa inaendelea kueleza, kuvutiwa na Kristo, kama alivyokuwa Mtakatifu Stefano, ina maana ya kuyafunua maisha katika mwanga wa wito wake, ni kufanya mabadiliko na kuongoza katika njia ya wema na ubinadamu kama upendo wa Mungu unavyotufundisha. RealAudioMP3








All the contents on this site are copyrighted ©.