2012-12-25 16:09:05

Hakuna sababu ya kupoteza tumaini - kwa kuwa ukweli umezaliwa - Papa


Baba Mtakatifu Benedikto XV1, katika ujumbe wake kwa jiji la Roma na dunia kwa ujumla"Orbi et Urbi, amehimiza watu kujenga tumaini la amani hata katika hali ngumu na hatarishi, kwa kutegemea ukweli uliozaliwa Bethlehem pangoni. Veritas de terra orta est!"
Papa amesema, Wapendwa ndugu zangu wake kwa waume, wakazi wa jiji la Roma na duniani kote, Krismasi Njema kwenu nyote na familia zenu.
“Katika Mwaka huu wa Imani, ninapenda kutoa salaam zangu za mataishi mema ya Noel, kwa maneno kutoka ya Zaburi: "Ukweli unachipuka katika nchi". Na kufafanua, hasa , katika ukweli wake , Mzaburi, alilenga katika siku zijazo:ambamo "Wema na ukweli vitakutana; / haki na amani vitakumbatiana / Ukweli atachupuka nje ya nchi, / na haki itaangalia chini kutoka mbinguni. / Bwana mwenyewe atawapa mafao yake; / nchi yetu itaongeza matunda yake. / Haki itakwenda mbele yake / na wokovu, sambamba katika njia ya hatua zake "(Zab 85:11-14).

Leo maneno haya ya kinabii yametimia . Kwa Yesu, kuzaliwa Bethlehem na Bikira Maria, wema na ukweli hakika vimekutana, haki na amani vimekumbatiana; ukweli umejichomoza kutoka katika nchi na haki imetazama chini kutoka mbinguni.
Papa pia amerejea maelezo ya Mtakatifu Augostine, anaye toa jibu fupi la kustaajabia, "Ukweli ni kitu gani? Ni Mwana wa Mungu. Na je, ni nchi?Ni mwili. Kwa kujiuliza Jinsi Kristu alivyozaliwa, utaona ukweli kwamba, ukweli umejitokeza katika nchi ... Ukweli Umezaliwa na Bikira Maria "(Zab 84:13 ) Veritas de terra orta est!"
Papa ameendelea kusema, katika Ibada ya Noel, Siku Kuu tunayo sherehekea kila mwaka, kwa ajili ya kutimizwa kwa unabii: 'ukweli ulio jichomoza katika nchi, na haki kuangalia chini kutoka mbinguni'. Ukweli, ambayo ni kiini cha Baba, umejitokeza duniani , kupitia tumbo la mama. Ukweli unaotawala dunia, umechipuka duniani, na kushikwa katika mikono ya mwanamke ... Ukweli ambayo mbingu haziwezi kuuzuia, umejichomoza katika nchi, na na kulazwa horini.
Je ni kwa faida ya nani Mungu Mkuu, kuwa hivyo mnyenyekevu? Hakika si kwa faida yake mwenyewe, lakini kwa faida yetu kubwa, iwapo tunaamini.

"Kama tunaamini, tutaiona nguvu ya imani . Mungu ametimiza kila kitu; amefanya hata lisilo wezekana , kuwa mwili. Uweza wake wote Mkuu wa upendo , umekamilisha jambo linalo pita ufahamu wote wa binadamu , milele kuwa mtoto na kuingia katika familia ya binadamu. Na bado, Mungu huyo , hawezi kuingia ndani ya moyo wangu kama sita mfungulia mlango. Porta fidei! mlango wa imani! Tunaweza kutishwa na hili , kutokana na udhaifu wetu wa kibinadamu. Kwa ubiandamu, kufungamana na Mungu, inaweza kutuogofya. Lakini kwa kuona hali halisi, hukimbiza mbali hofu na kuwa na tumaini linaloshinda woga. Kweli imejitokeza! Mungu kazaliwa. Nchi imezaa matunda (Zab 67:7).
Ndiyo, kuna ardhi nzuri, ardhi yenye rutuba, nchi iliyo huru katika yote, ubinafsi na ukosefu wa uwazi wote. Katika ulimwengu huu kuna udongo mzuri ambao Mungu aliuandaa, ili apate kuja kukaa miongoni mwetu. Makao ya uwepo wake katika dunia. Hii nchi nzuri, ipo hata leo, mwaka huu 2012, kutoka nchi hii , ukweli umejitokeza. Hivyo, kuna matumaini katika dunia, matumaini tunayo weza kuamini, hata katika nyakati ngumu sana na katika hali ngumu zaidi. Ukweli umezaliwa kwa ajili ya kuleta matumaini , wema, haki na amani.

Papa ametolea sala yake ili amani iweze kujichipuka kwa watu wa Syria, ambao mioyo yao imepondeka na migawanyiko inayosababishwa na mizozo isiyojali hata watu wanyonge wasioweza kujitetea wenyewe na kuvuna waathirika wasio na hatia. Kwa mara ingine Papa ametoa ombi kwa wahusika wote kusitisha umwangaji huo wa damu , na kuruhusu pia huduma na misaada kuwafikia wakimbizi na watu waliokimbia makazi yao ya kudumu . Papa Pia amewaomba wanasiasa waketi chini pamoja ili kupata ufumbuzi wa kisiasa unafaa kusitisha mgogoro huo.

Amani na ichomoze katika Nchi ambapo Mkombozi alizaliwa, na kuwapatia Waisraeli na Wapalestina ujasiri mkuu, kumaliza migogoro na migawanyiko ya miaka mingi, na ili waweze kutembea katika njia ya majadiliano.

Na kama ilivyo katika mataifa ya Afrika ya Kaskazini, ambako tunashuhudia , hatua kubwa katika mapito kwa ajii ya hali ya siku zijazo , na hasa kwa taifa pendevu la Misri , lililo pata kubarikiwa na utoto wa Yesu – Watu na waweze kufanya kazi kwa ushirikiano na mshikamano , kwa ajili ya kujenga jamii iliyosimikwa katika misingi ya haki na heshima kwa uhuru na hadhi ya kila mtu.

Amani na ichupuke katika bara kubwa ya Asia. Mtoto Yesu na alitazame kwa macho yake ya neema, wakazi wa nchi hizo na, kwa namna ya pekee, kwao wote wale wanao mwamini Yesu. Mfalme wa Amani, na awageukie viongozi wapya wa Jamhuri ya Watu wa China ambao majukumu makubwa yanawasubiri. Ni matumaini yangu kwamba, wataweza kutimiza kazi hii, kwa namna ambamo wanaweza kusaidia kujenga jamii ya kidugu kwa manufaa ya watu wote wa taifa heshimiwa la China na duniani kote.

Kuzaliwa kwa Kristu na kuwezeshe kurudisha amani Mali na mapatano nchini Nigeria, ambako ukatili wa kighaidi, unaendelea kuvuna waathirika, hasa miongoni mwa Wakristo. Pia Mkombozi aweza kuwa msaada na faraja kwa wakimbizi kutoka mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na amani nchini Kenya, ambako kumekuwa na mashambulizi ya kikatili kwa raia na katika maeneo ya kuabudu.

Mtoto Yesu na abariki idadi kubwa ya waamini wanao shereheka naye katika mataifa ya Amerika Kusini. Na awaongezee fadhila za kuthamini binadamu na tunu za kikristo, zidumu kwa wale walazimishwa kuondoka au kuwa mbali na familia zao na nchi yao, na pia awaimarisha viongozi wa serikali katika dhamira yao ya kufanikisha maendeleo kw awote na kukomesha uhalifu.

Papa amekalisha ujumbe wake akisema, Ndugu zangu, wake kwa waume! Wema na ukweli, haki na amani vimekutana, na kumwilishwa ndani ya Mtoto aliyezaliwa na Maria,horini Bethlehemu. Mtoto huyo ni Mwana wa Mungu; Mwana wa Mungu anaye onekana katika historia. Kuzaliwa kwake, ni kuchanua kwa maisha mapya kwa ajili ya binadamu wote. Naomba kila nchi, iwe nchi nzuri yenye kupokea na kufadhili wema na ukweli, haki na amani. Heri ya Krismasi kwenu nyote!








All the contents on this site are copyrighted ©.