Mapadre ni manabii na askari wa Kristo wanapaswa kuwa tayari kutekeleza utume wao
bila ya kujibakiza na kamwe wasimezwe na malimwengu!
Askofu mkuu Yuda Thadeus Ruwaich wa Jimbo Kuu la Mwanza, Tanzania, katika makala iliyopita
alitafakari kuhusu heshima na madai ya Manabii. Leo katika mwendelezo wa makala iliyopita
anagusia kwa undani zaidi kazi ya Nabii katika Ulimwengu mamboleo, kazi inayoendelezwa
na Mapadre wanaoshiriki ukuhani wa Kristo bila hata mastahili yao.
Hawa ndio
wanaoendelea kutoa mwaliko kwa waamini kutubu na kumwongokea Mungu, ili waweze kuonja
huruma na upendo wake usiokuwa na kifani uliopelekea hata akamtuma Mwanaye wa Pekee,
yesu Kristo kuja ulimwenguni kumkomboa mwanadamu kutoka katika utumwa wa dhambi na
mauti.
Askofu mkuu Ruwaichi anasema, Mapadre ni Askari wa Kristo wanaopaswa
kuwa tayari wakati wote kutekeleza yale yanayomhusu Mungu na Kanisa lake, kamwe wasimezwe
na malimwengu wakapoteza dira na mwelekeo wa maisha na utume wao katika ulimwengu.