2012-12-18 08:51:19

China na Vatican watiliana sahihi mkata wa ushirikiano katika sekta ya elimu ya juu


Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China imetiliana sahihi mkataba wa ushirikiano katika masuala ya kitamaduni na Vatican, tarehe 17 Desemba 2012. Pande hizi mbili zimebadilisha hati za makubaliano yaliyoridhiwa na pande hizi mbili.

Baraza la Kipapa la Elimu Katoliki litashirikiana na Wizara ya Elimu ya Serikali ya China katika masuala ya elimu ya juu pamoja na kutambua rasmi vyeti na shahada zinazotolewa na taasisi za elimu ya juu zinazomilikiwa na kuendeshwa na Kanisa nchini China.

Juhudi hizi zilifanywa na hatimaye kutiwa sahihi na Kardinali Zenon Grocholewski, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Elimu Katoliki na Dr. Wu Ching-ji, Waziri wa Elimu nchini China, hapo tarehe 2 Desemba 2011 na hatimaye kupitishwa na Bunge kwa kauli moja tarehe 20 Novemba 2012.







All the contents on this site are copyrighted ©.