2012-12-15 15:33:56

"Heri Wapatanishi", ni msisitizo wa Papa katika ujumbe wake kwa ajili ya Siku ya Amani Duniani.


Ujumbe wa Baba Mtakatifu kwa ajili ya siku ya Dunia ya Amani , unasisitiza Wajibu wa kuleta amani, na unahamasisha heshima kwa maisha ya binadamu
Kardinali Peter Kodwo Appiah Turkson, Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Haki na Amani pamoja na Askofu mkuu Mario Toso, katibu wa Baraza hili, Ijumaa waliwasilisha Ujumbe huo wa Papa Benedict XVI kwa ajili ya Siku 46 ya Amani Duniani, adhimisho litakalo fanyika tarehe Mosi Januari 2013. Ujumbe, emelenga katika mandhari ya tukio hili la kila mwaka: "Heri wapatanishi,".
Akiwasilisha ujumbe huo, Kardinali Turkson, alisema, kwanza inaweza kuonekana Kuwa ujumbe wa kinadharia, lakini yaliyotajwa, ndizo hali halisi zinazotendeka, katika ukweli.
"Ni wazi unaonyesha majukumu ya kuleta amani, ni lazima kulinda na kutetea heshima ya utu na 'maisha ya binadamu katika ukamilifu wake na katika vipimo vyote ya binadamu, ambamo huchota uangalifu wote makini na dharura za kupata suluhu kwenye matatizo kama vile maono sahihi wa ndoa, vipingamizi katika haki , uhuru wa dini, masuala ya kazi na ukosefu wa ajira, mgogoro wa chakula, mgogoro wa kifedha, na jukumu la familia katika elimu.
Hivyo ujumbe wa Papa , unatoa wito wa kuwa na mtindo mpya wa kiuchumi na kusitisha udikteta wa imani kwamba , maarifa na maaadili ni mambo ya mpito yanayotawaliwa na uwezo wa akili ya binadamu na wakati.
Papa anatoa ujumbe wake kama muhtasari mfupi wa Mafundisho Jamii ya Kanisa na mwongozo kwa Wakatoliki , kwa ajili ya ushiriki wa kijamii na kisiasa. Papa anatualika kuziishi heri nane za Injili, kwa ajili ya kujenga jamii yenye kuzingatia ukweli, uhuru, upendo na haki.
Papa anawaasa wale ambao wameishikila imani kwa Mungu na ahadi zake, huweza kuuona ukweli. Na kinyume chake, wale wasiokuwa na imani kwa Mungu, hujishaua wenyewe kwa kufanya mikakati yao ya binadamu, yenye kuwakosesha kuuona ukweli .
Bila Mungu, kwa kweli, hatima yake daima ni kutawaliwa na nguvu za kutaka faida, na hukaribisha mifumo yote ya dhambi : ubinafsi na ukatili, uchoyo na tamaa ya madaraka na utawala, kutovumilia, chuki na kudhulumu miundo.
Maelezo ya Papa, yanaonyesha kwamba, Amani ni sharti la kuvunja udikteta wa nadharia ya kufikiri kwamba, maarifa na maaadili ni mambo ya mpito yanayotawaliwa na uwezo wa akili ya binadamu. Mawazo hayo potofu katika dhana ya maadili ya uhuru kamili huzuia utambuzi muhimu wa asili ya maadili ya sheria iliyoandikwa na Mungu ndani ya dhamiri ya kila mtu. " Tu katika njia hii amani inakuwa inawezekana tena kuachana na doto hizo za amani ya bandia. Amani ya kweli ni "karama ya Mungu kwa mwanadamu." Amani Ni pamoja na Mungu, amani kwa mwenyewe, amani na mtu mwingine na kwa viumbe wote.
Papa anapendekeza mfumo mpya wa kiuchumi, uachane na nadharia za kutaka faida za harakaharaka kwa ajili ya manufaa binafsi lakini kutathmini hali za watu, katika uwezo wao wa kukidhi mahitaji licha ya ushindani. Mfumo mpya wa kimaendeleo uliosimikwa katika msingi wa udugu na kugawana, ufadhili na mantiki ya zawadi: ili kwamba kila mmoja ajisikie ni wajibu wake kujali mahitaji ya wengine, kwa kushirikiana na wengine katika mali zao. Ni kuuvua moyo wa ubinafsi,na kutambua kwamba katika kuwa daima na Mungu, binadamu anakuwa familia moja.
Papa ameendelea kutazama utendaji kwa ajili ya manufaa ya familia na haki ya kijamii, na dhamira ya elimu yenye faida ya kijamii akisema, ni muhimu kukuza na kueneza "mawazo, maneno na matendo ya amani"yaliyo jengwa katika mawazo na utamaduni wa amani, uaminifu, heshima, na urafiki. Haja kufundisha watu maana ya upendo na kuelimisha juu ya amani, na kuishi pamoja na wema katika hali za kuvumiliana.
Na pia kuwa walimu wa kutoa msamaha, na katika kujikatalia ulipizaji wa kisasi. Kuushinda ubaya kwa wema, na kuwa na" huruma, mshikamano, ujasiri na uvumilivu "Yote haya – Papa anasema si ndoto za kufikirika, lakini ni "polepole, yanakuwa ni mageuzi ya kiroho, elimu na maadili ya juu na dira mpya ya historia ya binadamu."
"Kanisa - amesema Papa – lina amini kuna haja ya kumtangaza upya Yesu Kristo, kwa sababu, kwanza, ni mkuu wa maendeleo kamili ya watu na pia ya amani." "Alama ya amani, kulingana na neema ya Yesu, ni moja ya sifa za atafutaye , maisha makamilifu ya kiroho na kimwili, leo na kesho”








All the contents on this site are copyrighted ©.