2012-12-14 15:10:56

Ujumbe wa Papa kwa Siku ya Amani Duniani, umewasilishwa


Ijumaa hii katika ukumbi wa Yohane Paulo 11, ndani ya jengo la habari la Vatican , kulifanyika Mkutano kwa wanahabari, kwa ajili ya kuwasilisha ujumbe wa Papa Benedikto XV1, kwa ajili ya adhimisho la 46 la Siku ya Dunia ya amani. Maadhimisho yanayofanyika kila mwaka tarehe Mosi January. Ujumbe wa Papa unaongozwa na Mada : Heri wapatanishi.

Kati ya walioongoza uwasilishaji wa ujumbe huo ni pamoja na Kardinali Peter Kwodo Appia Turkson , Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Haki na Amani. Pia Askofu Mkuu Mario Toso , Katibu wa baraza la haki na amani , na pia Flaminia Giovanelli , Katibu mwanandamizi katika baraza hilo .
Kardinali Turkson, akitoa maelezo katika mkutano huo amesema, kufuatia muonekano wa Baba Mtakatifu katika mtandao wa Twitter, imeonekana kuwa ni njia nzuri inayofaa zaidi katika kukutana na waandishi wa habari wengi zaidi, kuliko yalivyo mazoea ya kukutana ana kwa ana na wanahabari.

Papa kwa ajili ya adhimisho la Siku hiyo, amechagua kutafakari, moja ya Heri nane, za Hotuba ya Yesu ya Mlimani: "Heri wapatanishi. Kardinali anasema, "Ujumbe huo, unafungua wito mpya katika tukio la kustajaabisha katika maisha ya Kanisa, ambao ni Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, ambao hivi karibuni Mama Kanisa, alifanya maadhimisho ya kutimia miaka 50 ya uwepo wake.
Ni tukio linaloonyesha nguvu ya utume wa kanisa katika ulimwengu na majitoleo ya ya Wakristo katika historia ya mwanadamu .. Heri ya kiinjili na amani kama zawadi ya Mungu kwa mwanadamu, licha ya hali za kutisha katika ulimwengu wa utandawazi.








All the contents on this site are copyrighted ©.