2012-12-13 15:47:35

Papa akutana na Mabalozi wapya:ahimiza vijana kupata elimu si tu elimu dunia lakini pia muhimu kupata elimu ya kiroho.


Leo zaidi ya siku za nyuma, vijana wana haki ya kuelimishwa hisia za uwajibikaji na majitoleo, na serikali zinapaswa kutoa uhuru kamili katika elimu na katika kuwa mfano mzuri wa utendaji wa haki.
Ni maoni ya Baba Mtakatifu Benedikto XV1, kwa mabalozi wapya, wakati wakiwasilisha hati za utambulisho, Alhamis hii mjini Vatican. Mabalozi wapya wametoka Jamhuri ya Guinea, Niger, Zambia, Thailand, Sri Lanka na visiwa vya Saint Vincent na Grenadini, Magharibi mwa Indies.

Papa aliwashukuru kwa salaam za matashi mema kutoka kwa Marais na wakuu wa serikali wa nchi walizotoka, na pia kwamba wameteuliwa na kutumwa kwake, kwa ajili ya kutimiza majukumu yao, katika utumishi kwa manufaa ya watu wao. Aliwaombea Baraza zote za Mwenyezi Mungu ziwashukie wao na wafanyakazi wenzao ili waweze kufurahia maisha ya amani na kuheshmiana wakiwa wameungana katika umoja hapa Roma.
Hotuba ya Papa kwa Mabalozi hao, ikitazama changamoto nyingi za wakati wetu, imebaini kwamba, elimu inashika nafasi ya ya kwanza katika umuhimu. Na imetaja mchanganyiko wa katika dunia ya sasa ya utandawazi kwamba ni hali inayosababisha mabadiliko katika maisha na maarifa, na hivyo ikujenga uwezekano mkubwa wa mifarakano kibinadamu, kiutamaduni, kijamii na kiroho, na mno katika historia ya mwanadamu.
Papa ameitaja familia kuwa ni kituo cha kwanza cha kutoa elimu ya kuonekana iwapo itapandikizwa vyema akilini mwa watoto, kama msingi na asili inayopaswa kuendelezwa daima na kizazi kipya katika maana ya uwepo wao duniani. Aidha ni vivyo hivyo , katika maeneo ya elimu na mamlaka ya kielimu, ambamo walimu na wahadhiri, wanapaswa kuwa kioo cha ustaarabu na maisha adilifu.
Papa ameonyesha masikitiko yake kwamba, “ kwa bahati mbaya, umahiri wa baadhi yao umekuwa si kama wanavyotazamiwa, kwani kumekuwa na mwelekeo wa kuufinyanga ukweli na kutoa upendeleo fulani, hivyo kukosesha ufahamu halisi licha ya kuondoa au kupunguza ukweli kuhusu binadamu. Papa anakumbusha binadamu ni kiumbe muhimu, aiyeweza kuchukuliwa kijuujuu tu , kama mambo ambayo yanayoweza kuchezewa kama taka.
Papa ameasa, haki ya maadili ya elimu, kamwe isipuuzwe au kukataliwa. Na Wajibu ya kuelimisha maadili haya kamwe yasimezwe au kudhoofishwa na maslahi yoyote ya kitaifa au itikadi na kisera.
Papa ameitaja hiyo ndiyo sababu msingi ya kwa nini ni muhimu kuwaelimisha vijana katika ukweli na ukweli. Papa alimalizia hotuba yake kwa kuwaweka chini ya usimamizi wa Mama Bikira Maria , Mama wa Waheshimiwa wote. Na kwamba, idara za Jimbo Takatifu Curia ya Roma, zitakuwa wazi daima kutoa msaada kwao kila wanapohitaji. Na kwa furaha aliwapa baraka zake za kipapa wao na familia zao.








All the contents on this site are copyrighted ©.