2012-12-11 15:17:03

Uekumene katika moyo wa Uinjilishaji Mpya


Umoja wa Wakristu ni maluwiluwi au ahadi?:Matumaini ya Kiekumene katika mwaka wa Imani. Ni mada iliyoongoza Mhadhara wa Jumatatu katika Chuo Kikuu cha Lateran cha Roma. Mhadara huo uliogozwa na Mwanateolojia Kardinali Kurt Koch, Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya uhamasishaji wa Umoja wa Wakristu .

Katika tafakari yake, Kardinali Koch alisisitiza umuhimu wa kudumisha lengo la umoja kamili, lenye kuonekana kwa Makanisa kama njia pekee ya kutoa ushahidi wa kuaminika wa imani ya kikristo katika jamii ya leo, inayomezwa na mambo ya kidunia.

Kardinali Kuch akirudi katika madhari hii iliyojadiliwa hivi karibuni katika Mkutano wa Mwaka wa Baraza lake, alitaja tena umuhimu wa ekumeni katika moyo wa uinjilishaji wote mpya, kupambana na wazo la kisasa la malimwengu na ubinafsishaji wa dini, akibainisha kama sehemu ya matokeo ya kutisha ya mgawanyiko na migogoro michungu kati ya Makanisa ya karne ya 16 na 17.

Aliendelea kueleza, tangu Mkutano wa kwanza wa Dunia ya Kimisionari, uliofanyika Edinburgh mwaka 1910, imezidi kujionyesha kwamba, utoaji wa ushuhuda wa kweli wa Injili ya Kristu, utafanikishwa veyma zaidi iwapo Makanisa yataweza kuondoa utengano uliopo na kutembea pamoja kama wamoja.

Kardinali Koch pia alisisitiza umuhimu sala katika kutafuta umoja Wakristu: kama Yesu alivyoomba katika karamu ya mwisho alipokuwa na wanafunzi wake "na wawe wamoja ili kwamba, ulimwengu upate kuamini". Kwa njia hiyo, Wakristu wote leo hii, wanapaswa kuongozwa na yote mawili sala na ushuhuda wa matendo, kupitia njia ya mapatano na umoja kamili wa Mwili Mmoja wa Kristo.









All the contents on this site are copyrighted ©.