2012-12-10 10:47:24

Umuhimu wa Jumuiya ya Kimataifa kushirikiana kwa pamoja ili kupata suluhu ya kudumu Ukanda wa Sahel, Kaskazini mwa Afrika


Professa Roma Prodi, mwakilishi maalum wa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, kwenye Ukanda wa Sahel, Kaskazini mwa Afrika, hivi karibuni alitembelea na kufanya mazungumzo na maafisa waandamizi kutoka Umoja wa Mataifa wanaowakilisha mashirika mbali mbali katika ukanda huu, ili kuzungumzia kinzani zinazoendelea sehemu hizi.

Kwa pamoja wamejadili matatizo msingi yanayoukabili Ukanda wa Sahel na jinsi ya kukabiliana na changamoto hizi kwa kuunganisha na kuimarisha nguvu zao za pamoja ili kuhakikisha kwamba, misingi ya haki, amani na utulivu inadumishwa. Wamefanya upembuzi yakinifu kuhusu hali tete nchini Mali na jinsi ambavyo Jumuiya ya Kimataifa inavyoweza kuchangia katika mchakato wa kupata suluhu ya kudumu.

Kwa pamoja wamebainisha umuhimu wa kushirikiana ili kuweza kupata ufumbuzi wa kudumu wa migogoro iliyopo kwenye Ukanda huu, ili hatimaye, wananchi waweze kufurahia maendeleo endelevu.







All the contents on this site are copyrighted ©.