Jumapili, licha ya baridi iliyokuwepo katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro
Vatican, maelfu ya watu walikusanyika katika uwanja huo nyakati za mchana kusikiliza
hotuba ya Papa na kusali pamoja nae sala ya Malaika wa Bwana . Katika hotuba yake,
Papa alihimiza waamini kuiandaa mioyo yao na maisha yao ya kila siku, kwa ajili ya
ujio wa Bwana , kama alivyo himiza Yohane Mbatizaji katika Injili ya Luka. Aliizungumzia
sauti iliayo nyikani, akisema, leo hii inaililia jamii ya ulaji , inayopendelea kujilimbikizia
mali na vitu vya anasa, na kujifurahia maovu, badala ya kumcha Mungu na kuzishika
amri zake, . Kilio cha Yohane Mbatizaji jangwani, kinafundisha watu kuishi kwa njia
inayofaa , ili kwamba kipindi cha Noeli, isiwe tu kipindi cha furaha za nje , lakini
furaha ya ndani ya moyo, furaha ya kumpokea Mwana wa Mungu , mwenye kuleta furaha
na amani ya kweli kwa wanao mwamini.