Kanisa lahitaji mchango thabiti wa Waamini, Papa asisitiza ema..
Kanisa la Ulimwengu linatazamia na linahitaji moyo wa Kitume, mwamko, ukarimu na mchango
thabiti , usiokuwa na mbadala toka kwa waamini Marekani zote mbili Kaskazini na Kusini
. Baba Mtakatifu alieleza siku ya Jumapili jioni wakati akihutubia Makardinali, Maaskofu,
Mapadre, Watawa na walei kutoka Bara za Amerika Umati huo ulikusanyika katika
Kanisa kuu la Mtakatifu Petro , Vatican, kushiriki Ibada ya Misa , kwa ajili ya Ufunguzi
wa Kongamano la Kimataifa juu ya Kanisa. Kongamano lililoanza Jumapili hiyo 09 -11
Desemba kwa ajili ya kuadhimisha miaka 15 tangu kufanyika kwa Sinodi ya Maaskofu kwa
ajili ya Amerika, na Mwaka wa Imani