2012-12-05 15:15:32

Mwenye Heri Anuarite : Heshima ya Wanawake.


Katika kitogoji cha Isiro, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, eneo linalojulikana kwa myumba wa kisiasa, vurugu na mateso hasa kwa wanawake, hapo tarehe 1 Desemba 1964, alifariki Sista Marie Clementine Anuarite.

Mtawa huyu wa Usharika wa Masista wa Familia Takatifu ya Wamba, alitangazwa kuwa Mwenye Heri na Papa Yohane Paulo II tarehe 15 Agosti 1985, wakati wa ziara yake ya kichungaji Kinshasa, mji mkuu wa DRC.


Katika Mwaka huu wa Imani na shuhuda thabiti hata kama ni kukikabili kifo, na wakati huohuo kuwa tayari kusamehe watesi, kabla ya kutoa pumzi ya mwisho, Mwenye Heri Anuarite, bikira na shahidi, anakuwa mfano wa kufuata hasa katika mataifa ya Afrika, katika mtazamo na azma ya kuheshimu utu wa mtu , maridhiano na amani, kwa watu wote wenye mapenzi mema.


Mandhari hii ilihamasishwa katika Kipindi Jumamosi cha Afrofonia, Desemba 1, 2012, ambayo ni Siku Kuu ya Kilitulujia ya Mwenye Heri Anuarita. Kipindi kiliwasilishwa na Maria Josè Muando Buabualo wa Idhaa ya Kifaransa na pia mchango kutoka kwa Dulce Maria Araujo Évora, wa Idhaa ya Kireno wote wa Redio Vatican kwa Afrika, na Augustin Bita, mchungaji wa jumuiya ya Wakatoliki wanaotoka Kongo, ambao kwa sasa wanaishi hapa Roma.
Nyote mwaalikwa kusikiliza.













All the contents on this site are copyrighted ©.