Baba Mtakatifu Karibu kwenye Jukwaaa la Mtandao wa Kijamii, Utwitter pamoja nasi!
Rais Shimon Peres wa Israel ni kati ya watumiaji wa kwanza wa mtandao wa kijamii Twitter
kumwandikia Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, akimwalika kwa mikono miwili
katika mtandao wa twitter kwa kusema kwamba, katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni
uhusiano kati ya Vatican na Israel umeboreka kwa kiasi kikubwa na kwamba, kwa pamoja
wanaweza kutangaza misingi ya amani.
Ujumbe wa Rais Shimon Peres umeandikwa
kwenye akaunti ya Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita @pontifex ambayo hadi sasa
inaendelea kuzua gumzo kutoka sehemu mbali mbali za dunia. Wachunguzi wa mitandao
ya jamii wanasema kwamba, hadi sasa zaidi ya watu nusu millioni wamekwisha jiunga
kwenye akaunti ya Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita.