2012-12-01 16:41:37

Tahariri ya Padre Federico Lombardi- Saburi na tumaini la majilio


Tahariri ya Padre Federico Lombardi kwa wiki hii, imeangalishwa katika kipindi cha majilio, kipindi cha kusubiri kwa tumaini, licha ya matatio ya kiuchumi na ukosefu wa ajira .

Amesema , kwa mara ingine, kinaanza kipindi cha majilio, wakati wa saburi na tumaini tunaloliangalisha katika Siku Kuu ya Noel.

Na kwamba, dunia kamwe haikosi matatizo na hali ngumu zinazomgusa binadamu katika njia yake ya ubinadamu na imani. Kwa mtazamo wa haraka katika mazingira yanayotuzunguka, tunaiona hali hiyo.

Padre Federico Lombardi ameendelea kuzungumzia matatizo ya Kiuchumi na ukosefu wa ajira, yanayorarua maisha ya watu wengi na kuwakosesha tumaini kwa siku zijazo na kudumaza juhudi za kuanzisha miradi mipya.

Pia amegusia matatizo ya kijamii na afya kama ilivyoelezwa katika maadhimisho ya Siku ya Kupambana na madhulumu dhidi ya wanawake na Maadhimisho ya Siku ya Dunia ya kupambana na ukimwi. Si hivyo tu lakini pia kuna matatizo ya machafuko ya kivita na migongano kama ilivyo huko Syria , Mali, Nigeria, Mashariki mwa Congo, Somalia , Afghanistani, na Iraq. Pia jamii inakabiliana na hali za mivutano na wasiwasi kijamii na kisiasa, kama ilivyo huko Misri.

Mhariri anasema, katika hali hizo, si rahisi kuitambua taa ya matumaini, hata kama baadhi hazikosekani, kama ilivyo katika mazungumzo yanayoendelea kati ya serikali ya Cuba, na kati Colombia na waasi FARC, na kupigwa kwa kura juu ya Palestina na Umoja wa Mataifa, pengine ni msukumo wa kuanza kwa mchakato wa amani na kama matumaini halali.

Padre Federico Lombardi amekamilisha tahariri yake na maelezo kwamba, kwa kifupi, tunaishi kati ya changamoto, wasiwasi, na matumaini tete. Hivyo kipindi cha Majilio kinapaswa kutusaidia kujiuliza na kutafuta majibu kwa matumaini makubwa, na tusikubali kumezwa na ukosefu wa matumaini, badala yake tujawe na tumaini ya ubinadamu, katika kipindi hiki cha matarajio.

Padre Federico Lombardi ameweka tumaini lake katika Juhudi zote za tafiti za kisayansi , kidiplomasia na kisiasa katika kutafuta amani ya kijamii, ndani kitaifa na ya kimataifa, katika maana na mshikamano unaomulikiwa tu kwa kina na uogofu wa mtu , unao mwezesha kuwa mtendaji wa amani kama alivyosema Bwana. Lakini ili iwe hivyo , tunapaswa kuutulea muda wa kipindi hiki cha majilio katika sala na kazi .








All the contents on this site are copyrighted ©.