2012-11-29 14:13:56

SECAM inadhamiria kuanzisha Taasisi ya Imani, Utamaduni na Maendeleo!


Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Afrika na Madagascar, SECAM, katika Warsha iliyofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam, kwa kushirikiana na Baraza la Kipapa la Utamaduni, imeamua kuanzisha Taasisi ya Imani, Utamaduni na Maendeleo, wazo ambalo linatarajiwa kuridhiwa na Wajumbe wa SECAM watakapokutana kwenye mkutano mkuu wa kumi na sita, Julai, 2013, nchini DRC.

Warsha hii ambayo ilikuwa chini ya uongozi wa Kardinali Polycarp Pengo, Rais wa SECAM, imehudhuriwa pia na Askofu mkuu Barthelemy Adoukonou, Katibu mkuu wa Baraza la Kipapa la Utamaduni. Wengine walikuwa ni Kardinali Theodore Adrien Sarr, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dakar, Senegal ambaye ni Makamu wa kwanza wa Rais SECAM.

Washiriki wa Warsha hii wamechambua kuhusu majadiliano ya kitamaduni na kiimani Barani Afrika; fursa, changamoto na matatizo Barani Afrika katika mchakato wa maendeleo; utandawazi, usasa, utawala bora pamoja na sera za maendeleo kwa Bara la Afrika







All the contents on this site are copyrighted ©.