2012-11-22 15:45:29

Rais Michel Joseph Martelly wa Haiti akutana na Papa Benedikto XVI mjini Vatican


Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, Alhamisi, tarehe 22 Novemba 2012, amekutana na kuzungumza na Rais Michel Joseph Martelly wa Haiti, na badaye, ujumbe wake umekutana pia na Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican, aliyeongoza ujumbe wa Vatican katika mazungumzo hayo.

Viongozi wa pande hizi mbili wamezungumzia uhusiano mwema uliopo kati ya Vatican na Haiti. Wamejadili kwa namna ya pekee, mchango wa Kanisa nchini Haiti kupitia Mashirika yake ya misaada hasa katika sekta ya elimu, afya na huduma ya maendeleo endelevu kwa Jamii.

Rais wa Haiti amelishukuru Kanisa kwa jitihada za kufufua hali ya nchi hiyo iliyokuwa imeharibika vibaya baada ya kukumbwa na tetemeko la ardhi. Viongozi hawa wawili wanapania kwa pamoja kuendeleza ushirikiano baina ya Kanisa na Serikali kwa ajili ya mafao ya wananchi wa Haiti.







All the contents on this site are copyrighted ©.