2012-11-22 08:07:07

Papa asikitishwa na mashambulizi ya kivita yanayoendelea Ukanda wa Ghaza


Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, Jumatano, tarehe 21 Novemba 2012 baada ya Katekesi yake, ameonesha masikitiko makubwa kutokana na mashambulizi yanayoendelea kutokea huko Mashariki ya Kati. Anasema, anafuatilia matukio haya yote kwa wasi wasi na hofu kubwa kutokana na kuongeza kwa mashambulizi kati ya Israeli na Palestina, kwenye Ukanda wa Ghaza. Pamoja na kuendelea kusali, lakini anawajibika kukumbushia kwamba, vurugu na visisasi si suluhu ya matatizo wanayokabiliana nayo.

Baba Mtakatifu anapenda kutumia nafasi hii kuwaalika viongozi wa pande hizi mbili kurudi tena katika meza ya majadiliano, itakayositisha vita. Anawahimiza viongozi wa pande hizi mbili kutekeleza maamuzi ambayo yatasaidia kulinda na kudumisha amani ili kuondokana na mgogoro wa vita na hatimaye, kujikita katika jitihada zinazopania kudumisha amani na upatanisho.







All the contents on this site are copyrighted ©.