Maaskofu Katoliki Kenya wafanya uteuzi wa baadhi ya watendaji wake wakuu
Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya limemteua Sr. Esther Wangui Kimani kuwa Mratibu
mpya wa Mashirika ya Kipapa ya Utoto Mtakatifu nchini Kenya, uteuzi ambao utaanza
kutekelezwa hapo Januari 2013.
Sr. Kimani anachukua nafasi iliyoachwa wazi
na Sr. Jane Nugi wa Shirika la Consolata ambaye hivi karibuni amechaguliwa kuwa Mkuu
wa Shirika la Waconsolata na hivyo kulazimika kuhamia nchini Tanzania.
Baraza
la Maaskofu Katoliki Kenya katika mkutano wake, uliohitimishwa hivi karibuni umemteua
Mama Jacinta Kathamu Mutegi kutoka katika kitengo cha misaada Baraza la Maaskofu Katoliki
Kenya ili kuwa Katibu mtendaji, Idara ya Afya Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya, uteuzi
ambao unaanza mara moja. .
Wakati huo huo, Maaskofu Katoliki Kenya, wamemteua
Bwana Stephen Mwalyo Kituku aliyekuwa katibu mkuu mtendaji wa Shirika la Misaada la
Kanisa Katoliki nchini Kenya, Caritas kuwa Mkurugenzi wa muda wa Caritas, Kenya, kisheria.