2012-11-08 10:13:04

Ujumbe wa Mababa wa Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican kwa wasomi


Baba Mtakatifu Benedikto XVI, katika viwanja vya Mt Petro Mjini Vatican, mnamo tarehe 11Oktoba 2012 anapofungua Mwaka wa Imani utakaofungwa katika Sherehe ya Yesu Kristo Mfalme 2013 ametupatia ujumbe sisi wasomi na watafiti akirudia maneno ya Baba Mtakatifu Paulo VI. RealAudioMP3
Anasema, wapendwa enyi watu watafuta ukweli, watu wa kufikiri na wanasayansi, watafiti juu ya mwanadamu, dunia, historia na wote walio mahujaji katika kuuendea mwanga wa UKWELI. Mama Kanisa daima yupo kwa ajili ya kutimiza mapenzi ya Mungu, na hivi kutafuta ukweli, kuishi ukweli na kulinda ukweli huo. Ndiyo kusema kuwa makini, akizama katika ujumbe wa ukweli ambao amekabidhiwa toka kwa Kristo. Katika hilo Mama Kanisa huweka nguvu iliyojaa unyenyekevu kwa Roho wa ukweli.
Wapendwa wasomi na watafiti baada ya utangulizi huu, Baba Mtakatifu anatuambia sisi wasomi na watafiti akisema, njia yenu ni yetu, wala njia yenu si ngeni kwetu. Mama Kanisa ni rafiki wa wote na rafiki wa wito wenu kama watafiti na wasomi. Mama Kanisa yuko pamoja nanyi katika mahangaiko na matamanio yenu ya mafanikio, na wakati inapofaa na kuhitajika Mama Kanisa huwafariji katika kutofaulu kwenu na pale mnapokatishwa tamaa.
Kwenu ninyi wasomi na watafiti bado tunao ujumbe na ujumbe ndo huu: Endeleeni kutafiti bila kuchoka na bila kupindisha ukweli. Kumbukeni maneno ya mmoja wa marafiki zenu wakuu, Mt. Augustino anayesema, njooni tutafute, tukiwa na hamu ya kutafuta, na tutafute tukiwa na hamu ya kugundua zaidi.
Toka hamu ya kutafuta na kugundua ukweli katika upole na unyenyekevu kuna heri za Mungu. Si hilo tu bali, kwa wale wote ambao pamoja na kuwa na ukweli na kuutunza wanazidi kuwa wanyenyekevu kutafuta mbinu za kuufanya uwe wazi zaidi na kuweza kufikisha na kuushirikisha kwa wengine. Mama Kanisa aona heri kwa wale wote ambao hawajaona ukweli lakini wanazidi kuutafuta kwa moyo mkunjufu. Kwa jinsi hiyo Mama Kanisa anasema ingekuwa vema kutafuta mwanga wa kesho kwa kutumia mwanaga wa leo hadi kufikia ukamilifu wa mwanga wenyewe.
Baba Mtakatifu anatukumbusha sisi wasomi na wanasayansi juu ya kufikiri, yakuwa KUFIKIRI ni jambo nyeti, kwa hakika ni kazi, kwa maana hiyo ole wao wanaofunga macho yao makusudi, ili wasione ukweli! KUFIKIRI ni wajibu na hivi kama mmoja anatengeneza roho ya gizagiza kwa mbinu lukuku, akiifisha na kuifanya na kuifanya iwe na kiburi basi azama katika hatari kubwa! Kumbe yafaa daima kujiuliza ni Je, ni mwongozo upi ulio wa uhakika kwa wanasayansi na wasomi kwa ujumla zaidi ya kufikiri vizuri katika njia ya mwanga?
Wapendwa wasomi na wanasayansi, bila kupoteza muda Mama Kanisa anakuja kwetu kutupatia njia angavu ya mwanga fumbo, ambayo ni IMANI. Mwanga fumbo watoka kwake yeye aliye MKOMBOZI wa ulimwengu, Kristu mfufuka, anayesema daima “Mimi ni nuru ya ulimwengu, mimi ni njia, ukweli na uzima”
Baba Mtakatifu anaendelea kusema, maneno haya yakumbukeni, Sayansi yautumikia ukweli na imani yautumikia ukweli. Kuweni na uhakika katika imani rafiki mkuu wa akili na mang’amuzi. Jiendeleze katika kuupata mwanga wa imani ili uweze kuukamata ukweli, ukweli wote.
Mama Kanisa awatakia matumaini na mafanikio katika shughuli nyeti hiyo ya kutafuta na kusimamia ukweli ambao utakupatia uhuru na heri na Baraka za Mungu. Amina
Ujumbe huu wafikishwa kwako na Pd. Richard Tiganya, C.PP.S.








All the contents on this site are copyrighted ©.