2012-11-08 09:46:47

Salam na matashi mema kwa Rais Barack Obama kutoka kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani


Baraza la Maaskofu Katoliki litaendelea kusimama kidete kulinda na kutetea Injili ya Maisha, tunu msingi za maisha ya ndoa na familia pamoja na uhuru wa kidini. Maaskofu wanamwomba Rais Barack Obama wa Marekani kuendelea kujitoa kwa ajili ya wote wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii, hususan watoto ambao bado hawajazaliwa, maskini, wageni na wahamiaji pamoja na kuhakikisha kwamba, anakabiliana kwa nguvu, hekima, nidhamu na utashi mkubwa changamoto zilizoko mbele ya wananchi wa Marekani.

Ni maneno ya Kardinali Timothy Dolan, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani, katika ujumbe wake wa pongezi na matashi mema kwa Rais Barack Obama kwa kuchaguliwa kwake kuwaongoza Marekani kwa kipindi kingine cha miaka minne.

Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani linamwombea Rais Obama ili aweze kutekeleza wajibu wake kwa kutafuta kwanza kabisa mafao ya wengi na kwamba, mijadala inayofanyika nchini humo, itazingatia heshima na upendo kwa kila mmoja, badala ya matumizi mabaya ya majukwaa kama ilivyojitokeza kwa siku za hizi karibuni. Mwishoni, wanamtakia kila la kheri na baraka tele Rais Obama na Makamu wake Biden, wakati huu wanapoanza kuwaongoza Wamarekani kwa awamu ya pili.







All the contents on this site are copyrighted ©.