Rais Baraka Obama aibuka kidedea katika kinyang'anyiro cha Urais Marekani
Baada ya patashika nguo kuchanika, katika kinyang’anyiro cha kuwania kwenda Ikulu
Marekani, Rais Baraka Obama amembwaga mpinzani wake Mitt Romney na hivyo kufanikiwa
kuingia Ikulu kwa mara ya pili. Rais Obama amemshukuru pia mpinzani wake kwa changamoto
kubwa alizozionesha hadi dakika ya mwisho ya kampeni za uchaguzi ambazo zimegharimu
takribani dolla billioni moja za kimarekani. Amewashukuru wapiga kura wake ambao wamemwezesha
tena kurudi Ikulu kwa kipindi kingine cha miaka minne. Masuala ya uchumi na maendeleo
ya wananchi wa Marekani ni kati ya mambo yaliyopewa kipaumbele cha kwanza wakati wa
kampeni ya vuta nikuvute nchini Marekani.